Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja amekagua ujenzi wa Hoteli ya Kitalii ya nyota tatu katika eneo la Lubambangwe Burigi Wilayani Chato kwa lengo la kuangalia maendeleo ya ujenzi wa hoteli hiyo inayotarajiwa kutumika kwa ajili ya watalii watakaotembea maeneo ya vivutio vya Utalii Wilayani humo.
Amefanya ziara hiyo ya kushtukiza jana kutokana na kusuasua kwa ujenzi wa
hoteli hiyo.
Mhe. Masanja amemuelekeza Mwakilishi wa Mradi huo kutoka TANAPA,
Jeremiah Machibya kumsimamishia mkataba mkandarasi huyo kama ameshindwa
kumaliza kazi kwa muda unaotakiwa.
"Kama mkandarasi kazi imemshinda tengueni
mkataba muweke anayeweza kuimaliza kazi hii kwa wakati" Mhe. Masanja
amesisitiza.
Mradi huo wenye gharama ya shilingi Bilioni 11 unaosimamiwa
na TANAPA ulianza mwezi Aprili 2020 na ulitarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2021
lakini mkandarasi ameongezewa muda hadi mwezi Machi, 2022 na gharama za ujenzi
zilizotumika mpaka sasa ni Bilioni 4.1.
No comments:
Post a Comment