Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimsikiliza Mkurugenzi wa banda la Ethiopia, Bi. Haimanot Kassave (kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu bidhaa zinazopatikana katika banda lao kwenye Maonesho ya Dunia ya Expo 2020 Dubai. Kushoto ni Mkurugenzi wa Diplomasia ya Uchumi, Balozi Edwin Rutageruka
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) leo Desemba 16,2021 ametembelea mabanda ya nchi za Uganda, Burundi, Ethiopia na Kisiwa cha Malta kwa lengo la kujifunza namna ambavyo nchi hizo zimeshiriki katika maonesho ya Expo 2020 Dubai.
Katika ziara hiyo, Mhe. Mary Masanja aliongozana na Mkurugenzi wa Diplomasia ya Uchumi, Balozi Edwin Rutageruka, Mkurugenzi wa Banda la Tanzania kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Bi. Getrude Ng’weshemi kutoka TanTrade na Afisa Masoko Mkuu kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Michael Makombe
No comments:
Post a Comment