Na Massoud Hamad, BLW
Wajasiriamali
kisiwani Pemba wamesema hatua ya serikali kuwasaidia kuwapatia mikopo
kumewawezesha kusongesha mbele maendeleo endelevu na kupunguza umaskini
kisiwani humo.
Wamaeeleza hayo kwa nyakati tofauti wakati walipotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Uchumi ya Baraza la Wawakilishi kujionea namna wajasirimali hao walivyoweza kunufaika na mikopo hiyo.
Wamesema kupitia mikopo wanayopatiwa ambayo haina vikwazo vikubwa imewawezesha kubuni shughuli mbali mbali za kiuchumi na kutoa ajira kwa vijana wengine kupitia miradi waliyoianzisha ikiwemo ya kilimo, ufugaji na biashara.
Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Kazi Uchumi Na Uwekezaji Mhe Mudrik Ramadhan Soraga amesema kutokana na hatua kubwa za maendeleo ya wajasiriamali hao kupitia mikopo hiyo ipo haja ya kuwaongezea ili kuweza kuwagusa watu wengi zaidi.
Nao wajumbe wa Kamati ya Uchumi chini ya Mwenyekiti wake mhe Sabiha Fil fil Thani wameishauri wizara kuendelea kutoa kipaombele cha kuwapatia mikopo na vitendea kazi wajasiriamali ambao wanafanya shughuli zenye tija ili waweze kurejesha kwa wakati na kuwanufaisha wengine.
No comments:
Post a Comment