Habari za Punde

Balozi wa Norway nchini afanya mazungumzo na Waziri wa Afya Mhe Nassor Mazrui

Waziri wa Afya , Ustawi wa Jamii,Wazee Jinsia na Watoto Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, akizungumza na Balozi wa Norway Elisabeth Jacobsen kuhusu kuendelea kuwasaidia katika Masuala ya Afya , mazungumzo hayo yalifanyika katika Wizara hiyo huko Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar , wakati Balozi huyo alipokuja Kumtembelea Waziri Afya.

Waziri wa Afya , Ustawi wa Jamii,Wazee Jinsia na Watoto Mhe. Nassor Ahmed Mazrui,akimkabidhi zawadi ya Kitabu chenye historia ya Zanzibar ndani yake  Balozi wa Norway Elisabeth Jacobsen, wakati alipokuja Kumtembelea Waziri huyo Wizarani kwake Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar, na kumuahidi kuletawatafiti kutoka Norway kufanya Utafiti katika masuala ya Afya za dawa na Miti shamba.

   (PICHA NA MARYAM KIDIKO – HABARI MAELEZO.)

Na Kijakazi Abdalla                 Maelezo  

 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema  itathamini misaada mbalimbali  inayotolewa na Serikali ya Norway hasa katika  nyanja ya afya na ustawi wa jamii.

Hayo ameyasema Waziri wa Afya,Ustawi wa Jamii,Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui huko Ofisini kwake Mnazimmoja wakati akizungumza na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Elisabeth Jacobsen.

Amesema Serikali ya  Norway  inaingiza fedha nyingi katika miradi ya kimataifa ambazo zinasaidia katika nyanja mbalimbali ambayo inasaidia wazee, wanawake na watoto .

Aidha Waziri Mazrui amemuomba Balozi wa Norway kuipatia Zanzibar Mashime ya kuangalia Saratani ya matiti kwa Wanawake ambayo maradhi hayo yanaathiri sana .

Nae Balozi wa Norway Nchini Tanzania Elisabeth Jacobsen amesema Serikali yake itaendelea kutoa misaada kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar hasa kuchukua tahadhari ya wazee na wanawake.

Aidha amesema Serikali yake itateta watafiti ili kuona kwamba wazanzibar wanafanya tafiti  za afya na matumizi ya dawa za miti shamba.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.