Mkulima wa viungo Aviwa Ali Songora mkaazi wa Kizimbani akielezea kuhusu kilimo cha vanilla anachoendelea kukilima mara baada ya kupata elimu kutoka kwa shamba darasa kupitia mradi wa viungo unaofadhiliwa na jumuiya ya Nchi za Ulaya kupitia programu ya Agri-connect wakati alipotembelewa na watendaji wa mradi huo kuangalia Maendeleo ya mradi,Bi Aviwa anamiliki shamba la ekari tatu Kizimbani likiwa na mivanila 800 akikabiliwa na uhaba wa maji ya kumwagilia.
Afisa kilimo katika mazao ya viungo Community Forest Pemba (CFP)Ali Said Juma akitoa maelezo kuhusu lengo la mradi wa viungo unaofadhiliwa na jumuiya ya Nchi za Ulaya kupitia programu ya Agri-connect wakati wa ziara ya kuwatembelea wakulima wa shamba darasa kuangalia Maendeleo ya miradi na changamoto zinazowakabili, ziara hiyo ilianzia Kwa wakulima wa Bustani za nyumbani (kitchen garden)Kijichi ,wakulima wa viungo Kizimbani na Kiboje Muembeshauri na kumalizikia shamba la mbogamboga Kivunge .
Mkulima wa shamba darasa Kiboje Mwembeshauri Jaribu Mwinyi Khamis akielezea kuhusu kilimo cha hiliki wakati alipotembelewa na watendaji wa mradi wa viungo unaofadhiliwa na jumuiya ya Nchi za Ulaya kupitia programu ya Agri-connect kwa lengo la kuangalia Maendeleo ya mradi na kusikiliza changamoto zinazomkabili.
Mkulima wa bustani za nyumbani (kitchen garden)Salama Haji Juma mkaazi wa Kivunge akielezea faida anazozipata kutokana na kilimo hicho wakati alipotembelewa na watendaji wa mradi wa viungo kuangalia Maendeleo ya mradi na kusikiliza changamoto zinazomkabili,mradi wa viungo unafadhiliwa na jumuia ya Nchi za Ulaya kupitia programu ya Agri-connect.
PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment