Habari za Punde

Hatutamvumilia Mtu Yoyote Asiyelipa Kodi – Mwenda.

 

Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg. Yussuph Juma Mwenda akitoa maelekezo kwa wasimamizi wa Hotel ya The Residence iliyopo Mchangamle Mkoa wa Kusini Unguja. wakati wa ziara yake katika kutembelea Wafanyabiashara mbalimbali. 


Na. Mwandishi wetu.

Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg. Yussuph Juma Mwenda amesema kuwa ZRB haitamvumilia wala kumfumbia macho mlipakodi yeyote ambaye aidha halipi kodi au analipa viwango vidogo kinyume na uhalisia wa biashara yake inavyofanyika.

Ameyabainisha hayo wakati alipofanya ziara ya kikazi kukagua Hotel ya The Residence inayomikiwa na kampuni ya Hotel and Property ambayo ina hadhi ya nyota tano huko Mchangamle Mkoa wa Kusini Unguja.

Kamishna Mwenda amesema kuwa, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ina nia njema na Wazanzibari kwa kuwaalika wawekezaji kuja kuwekeza Zanzibar, hivyo kukamilika na kufanya kazi kwa miradi hiyo ya uwekezaji kuwe na ufanisi katika ulipaji wa kodi ili wananchi wapate tija kutokana na uwekezaji huo.

Aidha, Ndugu Mwenda ameueleza uongozi wa The Residence kuwa viwango vya kodi vinavyowasilisha ZRB na Hoteli hiyo haviridhishi, hivyo amewataka kuhakikisha kuwa wanaunganisha mifumo yao ya kibiashara pamoja na mfumo wa ZRB wa kutolea risiti za kielektroniki (VFMS) haraka iwezekanavyo ili kuondoa mianya ya upotevu wa mapato.

Kwa upande wa wasimamizi wa Hotel hiyo, wakiwakilishwa na Ndg. Diocles Ishengoma wamesema kuwa miundombinu ya barabara ambayo watalii wanaitumia kufika katika Hoteli hiyo sio rafiki jambo linalokwaza katika usafirishaji wa wageni.

Katika ziara hiyo, Kamishna Mwenda pia alitembelea ofisi za ZRB zilizopo Paje, na kuwaahidi watendaji walioko kituoni hapo kuwa uongozi utaiongezea uwezo ofisi hiyo ili iweze kuwahudumia walipakodi wote wa Mkoa wa Kusini Unguja kwa ufanisi.

Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg Yussuph Juma Mwenda akiongozana na maafisa kutoka ZRB wakiwa na Mwenyeji wao Ndg Diocles Ishengoma walipofika Hoteli ya The Residence kwa lengo la kukagua shughuli za biashara zinazofanyika katika Hoteli hiyo.


Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg Yussuph Juma Mwenda akikagua na kuangalia baadhi ya bidhaa katika duka liliopo ndani ya Hoteli ya The Residence iliyopo Mchangamle Mkoa wa Kusini Unguja.
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg Yussuph Juma Mwenda akikagua na kuangalia baadhi ya bidhaa katika duka liliopo ndani ya Hoteli ya The Residence iliyopo Mchangamle Mkoa wa Kusini Unguja.
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg. Yussuph Juma Mwenda akizungumza na mmoja kati ya walipakodi waliofika katika Ofisi ya ZRB Paje kwa lengo la kupata huduma.
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Ndg Yussuph Juma Mwenda akiongozana na maafisa kutoka ZRB wakiwa na Mwenyeji wao Ndg Diocles Ishengoma walipofika Hoteli ya The Residence kwa lengo la kukagua shughuli za biashara zinazofanyika katika Hoteli hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.