Habari za Punde

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan awasili Nchini Uganda kuanza ziara ya Kiserikali ya siku mbili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili Ikulu Entebbe nchini Uganda tarehe 10 Mei 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni wakati wa nyimbo za Taifa za Tanzania na Uganda zikipigwa katika mapokezi Rasmi kwenye Viwanja vya Ikulu vya Entebbe nchini Uganda.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Uganda kwa ajili yake mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Ikulu ya Entebbe nchini Uganda 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni wakati akisalimiana na Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Uganda mara baada ya kuwasili Ikulu Entebbe nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni wakati akiwasalimia Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Uganda mara baada ya mapokezi rasmi yaliyofanyika katika Ikulu ya Entebbe nchini Uganda
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwatambulisha Viongozi wa Taasisi mbalimbali kutoka Tanzania kwa Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Museveni wakati wa mapokezi rasmi yaliyofanyika katika Ikulu ya Entebbe nchini Uganda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Entebbe nchini Uganda
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni wakati wakielekea kwenye mazungumzo Rasmi katika Ikulu ya Entebbe nchini Uganda
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni katika Ikulu ya Entebbe nchini Uganda tarehe 10 Mei 2022.
PICHA NA IKULU.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.