Habari za Punde

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Mohamed Mussa Ahudhuria Mkutano wa "UN TRANSFORMING EDUCATION SUMMIT 2022" Paris.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe  Lela Muhamed Mussa akiwa katika mkutano wa  "UN Transforming Education Summit 2020" unaofanyika Paris Nchini Ufaransa. 

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Muhamed Mussa amehudhuria "UN TRANSFORMING EDUCATION SUMMIT 2022" huko Paris nchini Ufaransa.

Katika mkutano huo wa siku nne uliohudhuriwa na  mawaziri mbalimbali  duniani utajadili na kupitisha agenda mbali mbali kwa ajili ya mpango wa Elimu wa miaka mitano kwautakaotekelezwa na UNESCO.

Katika picha ni ya baadhi ya   wadau wa mkutano wa  wanufaika wa GPE  ikiwemo Tanzania bara na Zanzibar wenye lengo kuu la kuangalia jinsi nchi hizo zinavyonufaika na ufadhili wa GPE .

Kwa Zanzibar GPE imefadhili miradi mbalimbali kama Kusimamia uendeshaji wa Vituo vya Tucheze Tujifunze,
Kupatiwa vifaa vya kujifinzia na kufundishia, Kuwalipa maposho walimu wa vituo vya TuTu 
Kujenga, kukamilisha na kukarabati madarasa na vituo vya TuTu, 
Kuwapatia mafunzo ya kuinuwa kiwango  cha ufundishaji walimu wa madarasa ya Maandalizi na Vituo vya TuTu  na kuanzisha ujenzi wa vituo  vya TuTu kwa Unguja na Pemba.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe  Lela Muhamed Mussa akiwa na GPE Executive Director Charles North katika mkutano wa Wadau wa Wanufaika wa GPE ambapo ni muendelezo wa EDUCATION TRANSFORMATION PRE SUMMIT Paris Ufaransa.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.