Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, akimsikiliza Mfanyakazi wa Mfuko huo anayesimamia masyala ya uwekezaji.
NA
KHALFAN SAID, SABASABA
THAMANI ya Mfuko wa
Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) inakaribia trilioni 6 kulingana na mahesabu
ambayo bado hayajakaguliwa yaliyoishia Tarehe 30/6/2022, Mkurugenzi Mkuu wa
Mfuko huo, Bw. Masha Mshomba amesema.
Bw. Mshomba ameyasema
hayo kwenye Banda la NSSF kwenye Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar
es Salaam kwenye viwanja vya Julius Nyerere (maarufu Sabasaba) jijini Dar es
Salaam Julai 3, 2022.
“Kwa sasa tuko trilioni
5.8 hiyo ndiyo thamani ya Mfuko na thamani hiyo imekuwa ikikua sana kufuatia
mwitikio mzuri wa uchangiaji ambao
waajiri wamekuwa wakionyesha kwa takriban miaka miwili iliyopita” alisema
Akifafanua zaidi Bw.
Mshomba alisema, "tunavyozungumza sasa hivi makusanyo ya mwezi yanazidi
Bilioni 110.” Alibainisha.
Alisema mwaka ulioishia
tarehe 30/6 NSSF ilikusanya zaidi ya shilingi trilioni 1.3 (Trilioni 1 na
bilioni 300).
“Hili
ni ongezeko kubwa ukilinganisha na makusanyo ya mwaka uliopita ulioishia tarehe
30/6/ ambapo tulikusanya shilingi trilioni 1.1 (Trilioni 1 na bilioni 100),
ongezeko la zaidi ya asilimia 18% hii inatokana na kwanza kuwajengea mazingira
mazuri ya kazi watumishi yanayopelekea kuongezeka kwa ari ya kufanya kazi,
matumizi ya TEHAMA yanayoziba mianya ya utendaji kazi usio wa kuridhisha,
mwitikio wa waajiri na wafanyakazi,” Alifafanua.
Alisema Mfuko umekuwa
ukiwapa waajiri elimu ya Hifadhi ya Jamii hali ambayo anaamini imesaidia kuongeza
tija.
“Mtu
akielewa umuhimu wa Hifadhi ya Jamii swala la mchango linakuwa sio la
kumlazimisha kwasababu ndio njia pekee ambayo itampatia mtu kipato pale ambapo
uwezo wa kufanya kazi unapokoma, Hifadhi ya Jamii unaweza kuona kama ni jambo
dogo lakini umuhimu wake utauona unapofikisha umri wa miaka 60 ambao unastaafu
au kwa bahati mbaya umepata ulemavu na usiweze kufanya kazi.” Alisema.
Lakini kama umewekeza
kwenye Mfuko wetu mapato yako yako pale, watoto wako watapata, mwenza atapata
na ndio maana sisi NSSF tunasema tunajali maisha yako ya sasa na ya baadaye,
alisema.
Kwa upande wa ulipaji
Mafao, Mkurugenzi Mkuu huyo alisema mwaka jana NSSF ililipa Mafao shilingi
bilioni 594 na wanajiandaa kulipa shilingi bilioni 658 mwaka unaofuata ambapo ni
ongezeko la zaidi ya asilimia 10%.
“Mwitikio
ni mkubwa lakini tunaweza kulipa sana kwa sababu wanaoomba kulipwa Mafao ni
wengi lakini pia matumizi ya TEHAMA yanasaidia sana.” Alisema na kuongeza.. “Ndio maana tunasema siku za usoni sisi dhamira
yetu ni kuhakikisha kwamba tunatumia TEHAMA kwa matumizi yetu yote.
“Kiwango hiki sio kidogo, kodi hiyo inasiadia katika kuchangia maendeleo ya taifa ya ujenzi wa
miundombinu ya hospitali, shule.
Lakini pia NSSF imekuwa
ikisaidia jamii kupitia (Corporate Social Responsibility) ambapo alisema kuna
sera mahsusi inayowaelekeza kujikita katika mambao ya msingi kama vile Afya, Elimu,
Barabara na wamekuwa wakifanya kazi kubwa kupitia mpango huo.
Kuhusu ushiriki wa
Mfuko kwenye Maonesho hayo, alisema ni fursa nzuri ya kukutana na wadau ili
kutoa elimu ya masuala mbalimbali yahusuyo Hifadhi ya Jamii lakini pia
kuwahudumia wanachama na wananchi kwa ujumla.
Katika Maonesho haya tumekuwa
tukitoa elimu kuhusu Kikokotoo kipya.
“Tunatoa elimu ya
kutosha kuhusu mabadiliko ambayo yametokea katika sekta ya Hifadhi ya Jamii
kama mnavyofahamu kumekuwa na mabadiliko ya kikokotoo namna ambavyo tunawalipa
wastaafu wetu kuanzia tarehe 1/7/2022, tumebadilisha kidogo fomula ya ulipaji.
Jambo hili lilikuwa la
muda mrefu tangu serikali ya awamu iliyopita mwaka 2018 yalitoka maagizo ya
kulifanyia kazi suala hilo kwa kushirikisha wadau wa vyama vya wafanyakazi,
waajiri na serikali.
Uamuzi huo wa serikali
ni kufuatia malalamiko yaliyotokea baada ya ile fomula iliyowekwa kufuatia
mabadiliko ya sheria ya mwaka 2018
Tunashukuru kwa
jitihada kubwa zilizofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Samia Suluhu Hassan Jambo hilo limewezekana na kuanzia tarehe hiyo tuna fomula
mpya ya ulipaji Mafao.
Katika hili kwakweli
tunampongeza sana Mhe. Rais, jambo hili litabaki katika historia kama moja ya
Legacy yake, na nimpongeze pia Mhe. Spika Dkt. Tulia Ackson, Naibu Spika na
Wabunge kwa ujumla kwa kufanya kazi kubwa ya kulijadili swala hili kwa kina na
ninahakika Waheshimiwa Wabunge watakaporudi kwa wananchi huko majimboni
watakuwa wawakilishi wazuri sana kuwaelezea wananchi kuwa jambo hili lina umuhimu
mkubwa kwa taifa.
“Kufuatia mabadiliko
hayo NSSF sasa italipa malipo ya mkupuo asilimia 33% badala ya asilimia 25% ya
fomula ya zamani kwa hiyo ni jambo zuri na wananchama wamelipokea vizuri na
maisha ya wananchama yataendelea kuboreka.” Alisema.
Matumizi
ya Mifumo (TEHAMA)
Pia tunasisitiza sana
matumizi ya Mifumo ndani ya NSSF, takriban miaka miwili sasa tumekuwa tukitoa
kipaumbele shughuli zetu zote za msingi tunazifanya kwa kutumia mifumo, jambo
hilo ni muhimu kwa sababu kwanza linaboresha huduma lakini pia linatupunguzia gharama za uendeshaji na
wateja wamekuwa wakifurahia kwa sababu linawapa urahisi wa kufanya mambo yao na
wengi hawahitaji kuja katika ofisi za NSSF, huko waliko wnaaweza kutumia simu
zao au komputa wakaingia kwenye website ya NSSF na kupata huduma zetu bila ya
kuhitajika kufika ofisini kwetu.
Nijambo tulilolipa
kipaumbele na tunatumia maonesho haya kuzidi kuwaelkimisha wanachama wetu na
wananchi kwa ujumla kuhusu matumizi ya TEHAMA na tunawaahidi kwamba hata kwa
zile shughuli chache ambazo hazijawekwa katika mfumo, ndani ya mwaka mmoja huu
unaokuja tunatarajia kwamba tutakuwa tumeziweka katika mfumo na tunatumaini
tukifikia hatua hiyo huduma zetu zitaboreka sana na ndivyo dunia inavyokwenda
na sisi NSSF tunataka kwenda kidijitali na tunataka iwe ya kidijitali
kwelikweli.
TUNATOA HUDUMA ZA
KAWAIDA
Tuko hapo kwa ajili ya
kutoa huduma pia mtu akija kuulizia michango yake, akitaka kujua hatua ya mafao
yake yamefikia hatua gani
weze kulipwa, pia
akitaka kujisajili kama amekidhi vigezo tuko hapa kumsajili na vile vile
tunatumia nafasi hii kutatua kero wengine wakija si kwamba wanataka kuhudumiwa
tu lakini wanakuwa na kero zao kwa namna moja au nyingine tunatumia nafasi hii
kutatua kero kwa kadiri ambavyo mazingira yaliyopo hapa, kama yatashindikana
tutamuelekeza kushughulikia kero hiyo kwenye ofisi zetu.
UWEKEZAJI
Kutangaza shughuli zetu
za kiuwekezaji, kama mnavyojua NSSF ni moja ya taasisi kubwa hapa nchini
zinazowekeza kwa kiasi kikubwa sana, tunatumia nafasi hii kutangaza uwekezaji
wetu nyumba zetu za kupangisha na kununua mfano tuna nyumba huko Wilayani
Kigamboni hususan Mtoni Kijichi, Tuangoma, Dungu, maeneo ya Muongozo.
Tuna nyumba nzuri sana
na mwitikio wa kununua nyumba hizo umekua ni mzuri sana, pia tunajenga jengo la
Mzizima hapa Dar es Salaam na nia hasa ni
kulipangisha kwa watu watakaoendesha mradi wa hoteli pia Mwanza na lengo
ni hilo hilo kulipangisha kwa mtu atakayeendesha shughuli za hoteli, tunatumia
Maonesho haya kutangaza hizo nafasi ndani ya nchi lakini pia nje ya nchi ili
tuweze kupata wadau hao ili kuhakikisha tunapata wapangaji au kununua nyumba hizo.
No comments:
Post a Comment