Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi Azungumza na Kuwasalimia Wanbanchi na Kutangaza Siku ya Mwaka Mpya wa Kiislam (HIJRIA) Kuwa ya Mapumziko.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi  akizungumza na kuwasalimia Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislam baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Qubba Kwaboko Wilaya ya Mjini Unguja leo, 5-8-2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi.(kulia kwa Rais) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar.Mhe. Haroun Ali Suleiman, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa uliyofanyika katika Masjid Qubba Kwaboko Wilaya ya Mjini Unguja leo 5-8-2022.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi  akisalimiana na mmoja wa Kiongozi wa Masjid Qubba Kwaboko Wilaya ya Mjini Unguja Bw. Ali Hobe,  baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid hiyo na (kulia kwa Rais) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi. 5-8-2022


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imekubali siku ya Mwaka mpya wa Kiislamu (hijria)  kuwa ya mapumziko.                                                                                                                        

Alhaj Dk. Mwinyi amesema hayo katika salamu zake kwa Waislamu baada ya kukamilisha Ibada ya Sala ya Ijumaa iliofanyika Masjid Qubba Kwa Boko Mkoa Mjini Magharibi.

Amesema Dunia iniatambua Kalenda ya Hijria ambapo waislamu hupata fursa ya kuadhimisha mwaka mpya w akiislamu, hivyo akatumia nafasi hiyo  kuipongeza Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kuja na utaratibu wa kuadhimisha Kalenda hiyo.

Alhaj Dk. Mwinyi alisema Serikali imeridhia maombi ya waislamu ya kuifanya siku hiyo kuwa ya mapumziko kitaifa kama ilivyo siku ya mwaka mpya wa Miladia.

Aidha, Alhaj Dk. Mwinyi aliwataka waislamu kuzingatia kwa kina umuhimu wa kufunga siku ya Ashuraa, ikiwa ni funga yenye fadhila kubwa katika mwezi huu wa Muharam.

Nae, Katibu Mtendaji Ofisi ya Mufti wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume aliwataka waislamu kuendelea kumuombea Dua Rais Alhaj Dk. Mwinyi kwa kuwa ni kiongozi muadilifu na mwenye kutekeleza kwa vitendo ahadi alizoweka.

Mapema, Khatibu wa Sala hiyo ya Ijumaa, Sheikh Hija Suleiman aliwataka waislamu kuendelea kufanya amali njema na kuondokana na maovu, kwa kutambua kuwa mwezi huu wa Muharam ni miongoni mwa miezi minne mitukufu katika uislamu.

Alieleza kuwa kuna fadhila nyingi zinazopatikana katika mwezi huu wa Muharami, ikiwemo ile inayotokana na muislamu  kukuthirisha funga , ambapo  hupata malipo makubwa.

“Kuna fadhila kubwa kwa kufunga sikukuu hii ya Ashuraa, mja hufutiwa madhambi ya mwaka mzima uliopita”, alisema.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.