Na Mwashungi Tahir -Maelezo
Wananchi wametakiwa kutoa ushirikiano katika kutoa takwimu sahihi kwa makarani wa sensa watakapo fika kwenye kaya zao ili lengo Liweze kutimia
Hayo yamesemwa na masheha wa shehia mbalimbali za Unguja walipotembelewa na kikosi cha uhamasishaji wakati wakipatiwa mafunzo ikiwa ni muendelezo wa ziara zao za kutoa taaluma juu ya zoezi la sensa.
Wamesema, wananchi watakapotoa taarifa kwa usahihi, wataisaidia serikali kupanga mipango mbalimbali ya kimaendeleo nchini.
Wamesema taarifa hizo sahihi ndizo zitakazowezesha kupatikana kwa masuala ya afya, elimu na miundombinu mbalimbali kama vile barabara sambamba na taarifa za kaya juu ya watu wenye mahitaji maalumu.
Aidha, waliwatoa hofu wananchi kwamba taarifa watakazozitoa kwa makarani zitakuwa siri kwa ajili ya matumizi ya kitakwimu pekee.
Masheha hao pia wameahidi kuifanyia kazi elimu waliyopewa kuhusu sensa na kwamba watakuwa mabalozi katika kuwafikishia wananchi na kufikia lengo lililokusudiwa.
Kwa upande wa Waratibu wa mafunzo hayo ya masheha wamewasihi kwamba kuhakikisha kila mwananchi anashiriki katika sensa kwa maendeleo endelevu ya taifa.
Hata hivyo Waratibu hao wamewaomba makarani ambao watakaopatiwa jukumu hilo kukusanya taarifa kwa umakini wakati wa mchakato huo kwani takwimu hizo ndiyo dira ya maendeleo.
Nae Ofisa Habari Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Sofia Abdalla Ali, amewaomba masheha hao kuyafanyia kazi mafunzo hayo kwa lengo la kurahisisha majukumu kwa makarani wataofika kwenye kaya zao. Na amewataka kutoa mashirikiano kwa watendaji wa sensa watakapo fika kwenye shehia zao.
Vituo vilivyofikiwa na kikosi kazi hicho ni pamoja na Rahaleo, Regezamwendo, Dunga Kiembeni, Charawe na Ukongoroni.
No comments:
Post a Comment