Habari za Punde

Maendeleo Makubwa Yamepatikana katika Sekta ya Elimu Nchini Tangu Kutangazwa Elimu Bila Malipo Miaka 58 Ilyopita

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , akizungumza na wanafunzi na walimu wa Skuli za Mikoa mitano ya Zanzibar pamoja na wananchi mbali mbali huko uwanja wa Amaan Mjini Unguja katika maadhimisho ya miaka 58 ya kilele cha tamasha la Elimu Bila Malipo, yaliyofanyika leo tarehe 23,septemba.

Mhe. Othman alimuakalisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Na.Kitengo cha Habari OMKR 23.09.2022.

Rais wa Zanzibar na Mwenyikiti wa Baraza la Mapinduzi   Mhe. Dk. Hussein Mwinyi, amesema kwamba maendeleo makubwa yamepatikana katika Sekta ya Elimu nchini tangu kutangazwa elimu bila malipo miaka 58 ilyopita.

Mhe.Dk Mwinyi ameyasema hayo katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman  huko Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar katika  maadhimisho ya kilele cha Tamasha la kutimia miaka 58 ya Elimu bila malipo Zanzibar.

Mhe. Dk . Mwinyi amesema kwamba mafanikio hayo yametokana na matokeo ya juhudi za Serikali katika utekelezaji wa mkakati wake wa kuimarisha miundombinu ya  upatikanaji wa huduma hiyo ikiwemo ujenzi wa taasisi za elimu za ngazi mbali mbali.

Amefahamisha kwamba hatua hiyo imepelekea  kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu kwa watoto  katika ngazi mbali mbali bila ya ubaguzi wa aina yoyote sambamba na kuongezeka ujenzi wa  wa taasisi za elimu kama dhamira ya mapinduzi ya mwaka 1964 ya kuweka fursa sawa ya elimu kwa wote.

Aidha Mhe. Mwinyi amesema  Serikali awamu ya Nane, inaendelea kufidia michango ya elimu iliyokuwa ikitolewa na wazazi na wanafunzi wote wa skuli za Serikali za maandalizi hadi sekondari wanaendelea kupatiwa elimu bila kulipa na serikali ikizipatia skuli nyenzo na vitendea kazi kama vile chaki na madaftari.

Pia Mhe. Mwinyi amesema kwamba mbali na vifaa hivyo, skuli zote za sekondari za Serikali zinaendelea kupatiiwa fedha kulingana na idadi ya wanafunzi ili  kusaidia uendeshaji wa skuli hizo katika kipindi hiki ambacho Serikali imechukuwa hatua ya kufuta michango ya wazee maskulini.

Aidha amesema kwamba kutokana na juhudi za serikali kutimiza lengo la Elimu bila malipo, idadi ya skuli imeongezeka kwa kiwango kiukubwa ambapo maandalizi zimefikia 153 kutoka skuli moja kabla ya mapinduzi , wakati msingi hivi sasa zimefikia 577 na sekondari ni 228 kutoka tano kabla ya mapinduzi ya mwaka 1964.

Akizungunzia Vyuo Vikuu, amesema kabla ya Mapinduzi Zanzibar haikua na chuo Kikuu hata kimoja, lakini hivi sasa vipo vinne vyenye jumla ya wanafunzi  12,527  na pia ipo taasisi ya ufundi Karume na vipo vyuo vitano vya mafunzo ya amali  na vituo vya Elimu mbadala Unguja na Pemba.

Amesema shabaha ya serikali ni kutatua changamoto zote zilizopo katika sekta hiyo kwa kuongeza miundombinu ya kujifunzia na kufundishia ili kufikia azma ya serikali ya kuwa na wasomi wakaoweza kuongeza idadi ya wataalamu kila fani ili kusaidia  ujenzi wa nchi.

Kuhusu maslahi ya waalimu, Mhe. Mwinyi amesema Serikali imepandisha mishahara  ya walimu  kiasi ambacho hata walimu wenyewe hawakuamini ongezeko hilo na kuahidi kwamba Serikali itaendelea kuangalia maslahi ya wafanyakazi hao kadri uwezo  wa uchumi unavyoruhusu.

Akizungumzia Uchumi wa bluu Dk. Mwinyi amesema kwamba Serikali ya Awamu ya Nane inaendelea na azma yake ya kuisimamia kwa vitendo sera ya  Uchumi huo nili kutoa fursa kwa wananchi kuweza kunufaika na rasilimali za bahari.

Ameongeza kuwa, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ni wadau wakubwa wa kutoa elimu hapa nchini, kwa hivyo wana wajibu kuungana na Serikali kupitia taasisi mbalimbali kuhakikisha kuwa marekebisho ya Sera ya Elimu na Mitaala yanazingatia mahitaji ya Uchumi wa Buluu.

Amefafanua kwamba katika kuhakikisha hilo, Serikali hivi karibuni itaanza utekelezaji wa Mradi Mkubwa wenye lengo la kuimarisha Uchumi wa Buluu wa kuwaongeza ujuzi, maarifa na utaalamu vijana  katika Soko la Uchumi huo ambapo  utaongeza vyuo vya amali kote nchini, utajenga Chuo cha Ubaharia, na utaimarisha Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia.

Aidha Mhe. Mwinyi ametoa wito kwa waalimu kote nchini kwamba ongezeko la mishahara liwe chachu ya kuongeza bidii katika kutekeleza wajibu na majukumu, ili kuleta mabadiliko ambayo Serikali inakusudia.

Naye Waziri wa Elimu na Mafunzoya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhammed Mussa amesema  kwamba wizara hiyo itaendelea kusimamia malengo ya elimu bila malipo katika kuhakikisha kwamba kila mtoto wa Zanzibar anapata elimu anayostahiki.

Amsema kwamba ni busara kila mmoja kuhakikisha anashiriki kusimamia sera ya elimu bila malipo sambamba na kuangalia mwendendo wa dunia katika kuhakikisha kwamba elimu inafanyiwa mageuzi katika kuhakikisha elimu ya nchi inakwenda na mahitaji .

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Maunzo ya Elimu Ali Khamis  Juma amsema kwamba katika jitihada za serikali kuendelea kuimarisha sekta ya elimu na kufanya mageuzi katika sekta hiyo imeunda kikosi kazi na tayari kinafanya kazi kubwa ya kupokea  maoni ya wadau kuhudu haja ya mabadiliko katika elimu Zanzibar.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mjini Mgharib akitoa salamu za Mkoa Mkuu wa Wilaya ya Magharib ‘B’ Hamida Mussa Khamis kwa Niaba ya Mkuu wa ,Mkoa amesema kwamba Mkoa umeridhika na juhudi za kuatatua changamoto za elimu kwa kujenga miundombinu muhimu ikiwemo madarasa jambo ambalo litapunguza sana idadi ya wanafunzi madarsani hadi kufikia 45. 

Kilele cha Elimu bila Malipo kutimia mika 58 limeanza kwa tamasha la elimu elimu lilohusisha mashindano ya michezo mbali mbali  ikiwemo mpira wa miguu na utunzi wa isha pamoja na msaula kadhaa ya kitaaluma amba zawadi mbali mbali zilitolewa.

Aidha mapema mgeni rasmi alipokea maandamano ya wanamichezo wanafunzi kutoka Skuli mbali  za Unguja na Pemba kwa mikoa yote mitano ya Zanzibar.

Imetolewa  na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha Habari leo tarehe 23.09.2022.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.