MAKAMU wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema ni muhimu kwa
Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), kuangalia pengo la Kisera katika mfumo wa
ukusanyaji mapato nchini na kuufanyia mageuzi sahihi ili kuongeza ufanisi na kukuza kiwango
cha mapato Zanzibar.
Mhe. Othman
ameyasema hayo ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar, alipozungumza na
Kamshina wa ZRB ndugu Ramadhani Juma Mwenda aliyefika ofisini kwa Makamu kujitambulisha
na kubadilishana naye mawazo kuhusu masuala mbali mbali yanaoweza kuchangia
ufanisi na kukuza kiwango cha mapato yanayokusanywa Zanzibar.
Mhe. Makamu
amefahamisha kwamba yapo maeneo mengi ya Mapato ambayo yanaweza kufanyiwa
mageuzi zaidi ya kisera na kisheria
jambo litakalochangia kuongeza kiwango cha mapato yanayokusanywa kupitia vyanzo
tofauti vilivyopo nchini.
Aidha Mhe. Othman amesema hatua ya hiyo pia
itasaidia sana kuwepo vyanzo zaidi vya mapato yatakayoweza kuchangia kasi zaidi
ya maendeleo ya nchi kutokana na kiwango kikubwa zaidi cha mapato kuweza
kukusanywa.
Mhe. Othman
amesema kwamba yapo maeneo mengi ambayo baada ya mageuzi ya kisera na kisheria kufanyika
yataweza kutumika kukusanyia mapato zaidi na nchi ikaweza kuendelea kwa kasi kubwa kwa kiwangpo cha mapato yatakayopatikana
kuliko ilivyo sasa.
Pia Mhe.
Othman amesema kwamba kuna haja ya kuchambua zaidi viwango vya malipo vinavyokana na ushuru wa stamp
hasa katika kutafautisha mapato ya aina hiyo kupitia miradi mikubwa na inayoanzishwa nchini ile ya
kawaida ambapo viwango vyake vinaweza
kuwa tafuati kuliko ilivyo sasa.
Aidha
amesema kwamba kuna fursa nyingi za
mikopo ya kifedha katika mabenki mbali mbali nchini zinazoweza kutumika kibiashara lakini zimekuwa
zikitumika zaidi kwa bikopo ya watu binafsi
kuliko mashirika ambayo yanaweza kuwa
na kiwango cha tija zaidi katika kasi ya ukusanyaji mapato nchini.
Amefahamisha
kwamba pia eneo la utayarishaji wa mikataba ya kibisashara kupitia watu binafsi,
mashirika na taasisi nalo ni muhimu kuangaliwa kwani linaweza kusaidia kuongeza
kiwango cha ukusanyaji wa mapato na kuchangia kasi zaidi ya kukuza uchumi wa
Zanzibar.
Mhe. Othman
ameshauri pia katika jitihada za kuongeza kiwango cha mapato bodi hiyo
kuangalia uwezekano katika utaratibu wa Benki za Kiisalamu kwa kuwa bado
kunachangamoto kwenye eneo hiilo na itakapotatuliwa itachangia kiwango cha
mapato kuongezeka nchini.
Naye
Kamshida wa Bodi hiyo ndugu Ramadhani
Juma Mwenda, ameeleza kwamba ZRB inaendelea kufanya mageuzi katika
mifumo yake ya ndani ya
ukusanyaji mapato jambo linalochangia kuongeza kiwango cha mapato
yanayokusanywa Zanzibar kupitia bodi
hiyo.
Amesema
kwamba kutokana na hali hiyo
wamefanikiwa kuongeza kiwango cha ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha Mwezi Julai
hadi Septemba mwaka huu kimeongezeka
kutoka shilingi bilioni 131 hadi 135 kwa
kipindi cha miezi mitatu.
Amesema pia
jitihada kubwa imefanywa katika kudhibiti udanganyifu na uvujaji wa mapato sambamba na kutengeneza mazingira bora ya
ulipatiji kodi za aina mbali mbali jambo linalochangia
kuongeza ufanisi na mafanikio zaidi ya kukusanya kodi.
MWISHO
Imetolewa
na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar kupitia Kitengo cha Habari leo tarehe 17.10.2022.
No comments:
Post a Comment