Habari za Punde

Maafisa wa Habari na Mawasiliano wa Wizara na Taasisi Wakijadili Changamoto Kuhusu Utendaji wa Kazi Zao

Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Hassan Khatib Hassan akizungumza na Maafisa wa Habari  na Mawasiliano kutoka  Wizara  na taasisi  na  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  walioshiriki katika kikao cha Maafisa hao kilichofanyika katika ukumbi wa Radio Rahaleo Zanzibar.
Mwandishi Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar Raya Hamad akichangia jambo katika mkutano wa Maafisa wa Habari na Mawasiliano  katika kikao kilichofanyika ukumbi wa Radio Rahaleo Zanzibar.

Baadhi ya Maafisa wa Habari na Mawasiliano  kutoka Wizara na taasisi  za  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  wakimsikiliza Mkurugenzi (hayupo pichani) walioshiriki katika kikao cha Maafisa wa habari na Mawasiliyano kilichofanyika katika ukumbi wa Radio Rahaleo Zanzibar.

Picha na Miza Othman-Maelezo Zanzibar.

Na Ali Issa Maelezo 23/12/2022

Maafisa wa Habari na Mawasiliano nchini wametakiwa kutumia vyombo vya habari kwa  kutoa taarifa za utendaji wa kazi katika Ofisi zao  kwa lengo la kuihabarisha  jamii.

hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Habari Maelezo Hassan  Khatib Hassan wakati akizungumza na Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara tofauti katika ukumbi wa Sanaa, Rahaleo.

Amesema inapotolewa habari ya Wizara au Taasisi katika vyombo vya habari ,jamii itaweza kufahamu kinachofanyika katika Serikali yao na kusaidia kuonyesha ufanisi wa kazi

Amesema jambo hilo hupelekea kuonesha dhamira ya kweli kwani  kunamasuala mengi ya kimaendeleo yametekelezwa.

“Mengi mazuri yapo yaliofanywa na Serikali hivyo  ni vyema  kuyaonesha kwa kuandika ,” alisema Mkurugenzi.

Aidha alifahamisha kuwa kuwepo na ushirikiano na waandishi wa habari  pale ambapo wanapohitaji taarifa za Wizara au Taasisi  wazipate bila ya usumbufu.

 Hata hivyo aliwataka kuwa pamoja na Idara ya Habari Maelezo kwa kutuma taarifa zao pale ambapo kuna tukio la utekelezaji.

Nae Afisa Habari Muandamizi Salum Abdalla amesema  Maafisa Habari  ni watu muhimu katika kusimamia kazi za wizara au taasisi zao ikiwa ni moja ya majukumu yao .

  Hatahivyo aliwaeleza  Maafisa hao kuwa  karibu na Viongozi wa Taasisi zao ili kupata taarifa zinazotokea na kufahamu yaliopo.

Nae Afisa habari kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Kassim Abdi aliwafahamisha Maafisa hao kuandaa mpango kazi na kuuwasilisha katika vikao vya viongozi wao ili kupunguza changamoto zinazojitokeza katIka Wizara  au Taasisi zao .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.