RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewaomba wafanyabiashara
nchini kupunguza bei za bidhaa haswa vyakula kwa nia ya kuwapunguzia ukali wa
maisha wananchi wa kipato cha chini.
Dk. Mwinyi alitoa ombi hilo Ikulu, Zanzibar alipozungumza
na wafanyabiashara mbalimbali na kujadili kupanda kwa bei ya chakula nchini.
Alisema bidhaa za vyakula ikiwemo mchele zimepanda
maradufu hali iliyozusha taharuki kubwa kwa kuongeza ugumu wa maisha.
Alisema haijawahi kutokea mchele kupanda bei kiasi
kikubwa kama ilivyosasa na kuongeza kuwa ni bidhaa yenye uhitaji mkubwa kwa
wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba.
“Zanzibar mchele ndio kila kitu ni sawa na wenzetu
Arabuni ukiadimika unga, kukosekana mkate kunakuwa na vurugu mitaani, hapa Zanzibar
watu wetu tuu Rahimu sana, lakini sasa hivi wamefikishwa pabaya sana, kilo elfu
tatu mchele kubwa, haijahi kutokea, tujitahi Ramadhani inakuja na hili ni ombi
langu kwenu” Kwa hisia alitamka Dk. Mwinyi.
“Tukubaliane ndugu zangu wafanyabiashara hali ya
ndani sio nzuri, sisi tuone tabu mwananchi wa kawaida kununua mchele kwa kilo
shilingi 3000, mchele huu huu miaka miwili iliyopita sisi tunaingia madarakani
ilikua kilo shilingi 1700, leo tunakaribia mara mbili ya bei, inaumiza watu, pamoja
na bei nzuri ilioko bara tukubali kukosa iyo faida kwaajili ya watu wetu kwa
kipindi hiki tushushe bei ya ndani” Kwa hisia alizungumza Rais Mwinyi.
Alieleza kuguswa kwake na bei ya awali ya mchele na
kueleza hata kama isifikie ilikotoka kutokanana sababu mbali mbali za
mabadiliko ya kiuchumi lakini isiwe kwa bei ya 3000 ambayo ni kubwa sana kwa
wananchi.
Aliwashauri wafanyabiashara hao kushirikiana
kuchukua meli kubwa zitakazobeba zaidi ya tani 30,000 badala ya kuchukua meli
ndongo za tani 5,000 kwa nia ya kuwasaidia watu kuondokana na ugumu wa Maisha uliopo,
ilizingitiwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani unakaribia.
Aliwaeleza wafanyabiashara hao kuchukua meli kubwa
kutapunguza utitiri wa meli ndogo zenye kubeba tani kidogo hali aliyoieleza kwamba
inaongeza msongamano bandarini.
Kwa upande wao
wafanyabiashara walieleza changamoto kubwa iliyosababisha bidhaa kupanda bei ni
mkwamo wa utoaji mizigo bandarini pamoja na gharama kubwa za mizigo zinazotozwa
bandarini.
Aidha, waliiomba
serikali likiwemo Shirika la Bandari kufanya juhudi za ziada kupunguza mkwamo
wa utoaji mizigo na kutoa kipaumbele kwa bidhaa zenye mahitaji ya haraka kwa
wananchi ili kumpunguzia mzigo wa lawama Mheshimiwa Rais.
“Mzigo wa lawama kwa tatizo hili najua lote
unatupiwa serikali, wafanyabiashara tushirikiane kwa umoja wetu kupunguza hali
hii, wananchi hawaelewi nini kinaendelea lakini ukweli hasa bandari yetu
imezidia sasa mahitaji yameongezeka, lazima kutumiwe njia mbadala ya kuwahisha
mizigo, siku 30 nyingi sana mzigo kukaa bandarini” alisema Mfanya biashara
Bopar interprize.
IDARA YA MAWASILIANO - IKULU, ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment