RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewaagiza
watendaji wa taasisi za Umma kutekeleza kwa wakati maagizo yote yanayotolewa na
Serikali ili kujenga ufanisi wa majukumu yao.
Dkt. Mwinyi
alitoa maagizo hayo wakati akifungua Mkutano wa tano wa Baraza la Taifa la Biashara
Ikulu, Zanzibar.
Alisema ameunda
taasisi ya Ofisi ya Rais ya Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini,
(PDB) ili ifuatilie mambo yote yanayoamuliwa na Serikali kwa nia ya kuyapatia
suluhisho kwa wakati uliokubaliwa.
“Nimeunda
taasisi hii lengo ni kufuatilia utekelezaji wa mambo yote tunayoyaamua
serikalini” Alisisitiza Rais Mwinyi.
Alisema Uchumi
wa Zanzibar unakabiliwa na changamoto mbalimbali licha ya kuendelea kuboreka na
kueleza kuwa baadhi ya changamoto hizo ziko ndani ya uwezo wa Serikali kwaajili
ya kuzitatua na baadhi yao ziko nje ya uwezo kutokana na sababu za kiulimwengu.
Rais Dk.
Mwinyi alisema, athari za ugonjwa wa COVID 19 ziliathiri sana uchumi wa dunia
na mataifa mengi kutetereka kiuchumi haswa uchumi wa nchi za visiwa ikiwemo
Zanzibar.
Alisema licha
ya ugonjwa huo kupungua na kumalizika kwa baadhi ya mataifa lakini bado
umendelea kuyaandama mataifa mengine ikiwemo China ambae ni Mshirika mkubwa wa Maendeleo
kwa Uchumi wa Zanzibar.
Aliongeza
sekta ya usafirishaji bidhaa ni moja ya changamoto inayohujumu uchumi wa dunia
kutokana na sababu mbali mbali za kidunia na kueleza kuwa Zanzibar kwa kiasi
kikubwa imeathiriwa na changamoto hiyo mbali na ufinyu wa bandari ya Malindi, unaodhorotesha
huduma kwenye eneo hilo.
Akitoa
ufafanuzi juu ya ujenzi wa bandari ya Mpigaduri, Dk. Mwinyi alieleza, Serikali
ya awamu ya nane baada ya kuingia madarakani ilikuta tayari hatua za ujenzi wa
bandari hiyo zilikamilika kwa ajili ya ujenzi wa bandari ya makontena pekee
nakueleza kuwa Serikali ya awamu ya nane iliona haja ya mahitaji yaliyopo kwenye
bandari ya Malindi hayakidhi haja, ndio maana ilikuja na wazo la ujenzi wa
bandari ya Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja ambao utakwenda kuondosha
changamoto zote.
“Wakati
serikali ya awamu ya nane inaingia madarakani, ilikuta tayari mpango wa ujenzi
wa bandari ya Mpigaduri ulikuwepo kwaajili ya kuanzisha bandari ya makontena
pekee, hatua ya ujenzi huo ilifikia pazuri, lakini sisi tukaona tuzungumzie
ujenzi wa bandari kubwa wenye kukidhi haja zote” alifafanua Dk. Mwinyi.
Alisema
Zanzibar kwasasa inahitaji bandari yenye kukidhi haja zote ikiwemo bandari ya Makontena,
bandari ya mafuta, bandari ya Samaki na bandari itakayotoa huduma za kubeba
mizigo ya nafaka ikiwemo mchele na mambo mengine yenye uhitaji mkubwa, na
kueleza kwamba Mpigaduri pekee isingetosha.
Alisema Serikali
imefanya uamuzi wa ujenzi ya bandari ya Mangwapwani kutokana na kukidhi kwa
eneo kwaajili ya mahitaji yote pia alieleza kina kirefu cha bahari kwa eneo
hilo kinakidhi haja ya ujenzi na kuongeza kuwa Mpigaduri kutasaidia mahitaji ya
bandari ya Malindi ambayo kwasasa imezidiwa kutokana na ufinyu wa nafasi na msongamano
mkubwa wa huduma zinazotolewa.
Dk. Mwinyi
alifafanua ujenzi wa bandari ya Mangapwani utashirikisha sekta binafsi na kueleza
kwamba hautojengwa kwa fedha za mikopo.
Wakati huo
huo Rais Dk. Mwinyi
alizitaka Mamlaka za ulinzi ikiwemo Wizara yenye dhamana na Vikosi vya Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, Kusimamia utendaji wa Polisi Utalii kwa kuwafunza juu
ya kuwachunguza watembeza watalii na kuhakikisha kuwa wanavibali halali vya
kutembezea wageni kwaaajili ya usalama wa watalii, mali na maisha yao pamoja na
kuwaondoshea bugudha wageni.
Akiwasilisha taarifa ya Kamati
za Baraza la Taifa la Biashara, Katibu wa Baraza hilo ambae pia ni Katibu
Kiongozi wa Baraza la Mapinduzi, Mhandisi Zena A Said alieleza baraza lina
kamati nne ambazo ni Kamati ya Uchumi na Biashara, Uwekezaji na Kulipa kodi, Kamati
ya Kilimo Ufugaji, Uvuvi na Mazingira, Kamati ya Utalii na Kamati ya masuala ya
Ardhi.
Mhandis Zena alieleza Baraza
lilifanikiwa kuzifanyia kazi kwa kuzipatia ufumbuzi hoja mbalimbali
zilizowasilisjwa na kamati hizo miongoni mwao alieleza ni Maslahi ya
wanaopoteza ajira kwenye taasisi binafsi, Udhibiti wa wanaotembeza watalii
wasiorasmi, Udhibiti wa nyumba za kulala wageni, Maegesho ya magari yanayotumia
VAT, Athari za michezo ya baharini na Madai ya wakulima wa mbogamboga kwa
uchelewashwaji wa madeni yao kwa taasisi za Serikali.
Aidha,
Mhandisi Zena alieleza bahadhi ya mafaniko yaliyotokana baada ya kufanyiwa kazi
kwa hoja za kamati hizo alisema Kuanzshiwa kwa Fao la ukosefu wa ajira kupitia marekebisho ya
Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, (ZSSF) nambari 5 ya mwaka 2005, Kutungwa
kwa Sheria ya Mfuko wa huduma za Afya, Kuanzishwa kikosi cha Polisi Utalii na Diplomasia,
Kuanzishwa kanuni za kusimamia nyumba za kulala wageni, Kuanzishwa mfumo wa
ofisi Mtandao, Kuandaliwa mwongozo wa mahusiano baina ya wakulima na wamiliki
wa mahoteli Pamoja na kuundwa kwa bodi ya ushauri ya masuala ya ajira na
mishahara
Mkutano wa tano wa Baraza la
Taifa la Biashara uliofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa
Serikali wakiwemo Mawaziri wa Serikali, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi wa taasisi
za Serikali na Sekta binafsi.
Aidha, mada mbalimbali
ziliwasilishwa kwenye mkutano huo ikiwemo Muhtasari wa Sheria ya Baraza la
Taifa la Biashara la Zanzibar, Nafasi ya sekta binafsi katika kuchochoea ukuaji
wa uchumi wa Zanzibar na nyengine ambazo zilichangiwa na wajumbe waliohudhuria
mkutano huo.
No comments:
Post a Comment