Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Amekutana na Kuzungumza na Madaktabi Bingwa wa Moyo Kutoka Kuwait Ikulu Zanzibar

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Nchini Kuwait wa Taasisi ya “Children’s Heart Charity  Association” ukingozwa na Kiongozi wa Ujumbe huo Dr.Faisal Al Saedie (kulia kwa Rais) na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 11-2-2023.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimsikiliza Kiongozi wa Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Nchini Kuwait wa Taasisi ya “Children’s Heart  Charity Association” Dr. Faisal Al-Saedie (kulia kwa Rais) walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 11-2-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Nchini Kuwait wa Taasisi ya “Children’s Heart Charity  Association” ukingozwa na Kiongozi wa Ujumbe huo Dr.Faisal Al Saedie (kulia kwa Rais) na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 11-2-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Nchini Kuwait Dr. Faisal Al Saedie na Dr.Hesham Menshawy, wa Taasisi ya “Children’s Heart Charity Association ” ,baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 11-2-2023, Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema timu ya madaktari bingwa wa moyo waliopo nchini wakitokea Kuweit inatoa mchango mkubwa kwa Serikali katika kuwatumikia wananchi.

Alisema uwepo wa timu hiyo umeongeza nguvu za kiutendaji kwenye hospitali walizofikia madaktari hao na kueleza ni sehemu ya jitihada za Serikali ya awamu ya nane ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha sekta ya Afya nchini.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na timu hiyo iliyoongozwa na mwenyeji wao, Waziri wa Afya, Nassor Ahmed Mazrui.

Alisema tatizo la moyo bado linaendelea kuwasumbua wananchi wa Zanzibar na kueleza kuwa timu hiyo imekuja kutoa mchango zaidi kwa watoto wanaosumbuliwa na matatizo ya moyo.

Alisema bado kuna watoto wengi wanaokabiliwa na tatizo hilo na kuongeza kwamba timu ya madaktari hao anaamini itakuwa mchango mkubwa wa watoto wengi kupata matibabu wakiwa nchini.

Alisema Serekali imekua ikitumia gaharama kubwa ya matibabu ya moyo kwa kuwasafirisha wagonjwa nje ya nchi na kueleza mbali ya gharama za tiketi na matibabu ambazo wagonjwa na familia zao yanawagharimu lakini Serikali imekua ikibeba mzigo mkubwa kugharamia matibabu hayo.

Alisema Serikali ina lengo la kuona inatoa huduma zote nchini na kwamba magonjwa yote yanatibiwa ndani ya nchini bila ya kutumia gharama kubwa nje ya nchi ndio maana imejenga hospitali za kisasa kutoa wepesi kwa wananchi wake.

Dk. Mwinyi aliiahidi timu ya madaktari hao kushirikiana nao kwa kipindi chote watakachokuwepo nchini pamoja na kuwaasa kwamba wasisite kuiuomba Serikali endapo watakwama kwenye ufanisi wa kazi zao.

Alisema uwepo wa timu hiyo ni faida kubwa kwa Serikali pia aliwaomba mchango wao kiutendaji na kuendelea kuiunga mkono Serikali hasa kwenye hospitali zake mpya za Wilaya zilizojengwa ambazo zinahitaji wataalamu wa aina zote kuongeza nguvu ya kuwatumikia wananchi pamoja na kuwashauri kwenye masuala ya afya. Pia Dk. Mwinyi aliishukuru timu hiyo kwa kukubali kwao kufanyakazi na Serikali.

Naye Waziri wa Afya, Nassor Ahmed Mazrui, aliishukuru timu ya madaktari hao kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na kukubali kujitoa kuongeza nguvu kuimarisha sekta ya afya nchini.

Alisema timu ya madaktari hao kwa kushirikiana na madaktari wenyeji wa hospitali ya Mnazi Mmoja wamefanikiwa kuwahudumia watoto 33 waliokuwa wakisumbuliwa na matatizo ya moyo, 30 kati yao walitibiwa na kuruhusiwa kurejea majumbani mwao na watatu bado wanaendelea na matibabu hospitali hapo.

Mmoja wa Madaktari hao, Dk. Fesal Al - Said  akizungumza mbele ya Rais aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Afya, kwa mapokezi yao na ushirikiano inaowapatia tokea siku waliyofika nchini.

Alisema lengo la ujio wao Zanzibar ni kutoa ushirikiano kwenye kutatua matatizo ya watoto yanayowakabili hasa matatizo ya moyo.

Alisema taasisi yao ya kuwasaidia watoto wenye matatizo ya moyo kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo nchini kwaajili ya kutoa misaada ya matibabu kwa watoto hao.

Walisema lengo la taasisi yao ni kuokoa maisha ya watoto wanaosumbuliwa na matatizo hayo ili  kuwasaidia kufikia ndoto zao kwenye maisha yao ya baadae.

Hivyo, alishukuru ushirikiano wanaendela kuupata kutoka kwa wenyeji madaktari wenzao ambao alieleza ni wakupigiwa mfano.

Timu hiyo ya madaktari kutoka taasisi ya kuwasaidia watoto wenye matatizo ya moyo kutoka Kuweit imekuja na madaktari 40 wakiwa wamegawanyika wengine wapo Dar es Salaam na wengine Dodoma.

Nchi ya Kuweit ni taifa kutoka  Asia Magharibi ambayo inapakana na nchi za Iraq kwa upande wa Kaskazini, Saudi Arabia Kusini, pia inachangia mipaka ya bahari na nchi ya Iran.

IDARA YA MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.