Katika Mazungumzo hayo, Dkt.
Jafo amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na shirika hilo ya kusaidia mataifa
yanayoendelea ikiwemo Tanzania ya kusaidia miradi ya kukabiliana na athari za
mabadiliko ya tabianchi.
Amesema dhamira ya WFP ya
kusaidia katika upatikanaji na matumizi ya nishati mbadala itasaidia katika
kupunguza na kuzuia kasi ya ukataji miti kwa ajili ya kutafuta kuni na mkaa.
Aidha, Waziri Jafo amemuelezea
mwakalishi huyo namna Serikali inavyoshirikiana na wadau mbalimbali katika
kuhakikisha kupanda miti na kuitunza ili kupambana na ukame ambao unaweza
kusababisha wananchi kushindwa kulima na hivyo kukosa chakula.
Katika mazungumzo hayo pia
viongozi hao wamejadiliana kuhusu namna gani shirika hilo linaweza kusaidia
katika miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
“Sisi kama Tanzania
tunaendelea kushiriki katika mikutano ya COP (Mikutano na Mabadiliko ya
Tabianchi) inayofanyika kila mwaka katika nchi tofautitofauti, hayo ndio
matunda ya diplomasia ambayo Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu
Hassan ameikuza,” amesema.
Kwa upande wake Bi. Sara amepongeza
Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais inayosukuma mbele ajenda
ya utunzaji wa mazingira kwa shughuli mbalimbali ikiwemo zoezi la upandaji
miti.
Amesema kwa kuwa chakula
(mazao) na mazingira ni vitu vinavyoendana hivyo, wao kama WFP wako tayari
kuona Tanzania inafaidika na mikakati ya shirika hilo ya kusaidia katika
mapambano dhidi ya athari za madiliko ya tabianchi.
Pia Bi. Sara ameonesha dhamira
ya kushirikiana na Tanzania katika kutafuta teknolojia bora ya kupikia ambayo
ni rafiki kwa mazingira pamoja na kuunga mkono zoezi la upandaji wa miti katika
maeneo mbalimbali. Kikao hicho kimehudhuriwa pia na wataalamu Idara Mazingira
kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.
No comments:
Post a Comment