Habari za Punde

Maadili na Usalama Kazini Ndio Roho na Moyo wa Utumishi wa Umma

Na.Rashid Omar. -OMKR.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba kufuata maadili  na sheria za kazi kwa watumishi wote wa umma ni jambo muhimu katika maendeleo ya nchi kwa vile maadili na Usalama kazini  ndio roho  na moyo wa Utumishi wa umma katika nchi yoyote duniani.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko ukumbi wa Sheikh  Idrisa Abduli- Wakili  Kikwajuni mjini Zanzibar alipofungua mafunzo ya watumishi wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar kuhusu maadili ya kazi na usalama kazini.

Mhe. Makamu amefahamisha kwamba utumishi wa Umma Zanzibar umeanza miaka kadhaa iliyopita  kwa kupitia katika hatua mbali mbali na kwamba iwapo nchi inataka kujenga utumishi bora ni vyema pia kuangalia na historia.

Amesema kwamba Zanzibar wana kila sababu ya kuutunza na kuufanya utumishi wa umma utukuke  kutokana na historia yake iliyoanzia mwaka 1890 kwa kuanza mfumo rasmi wa serikali ambapo ndipo serikali ilipoanzishwa chini ya himaya ya utawala wa Kingereza na marekebisho yake sheria na kanuni hizo yakafanywa tangu 1906 na baadaye 1924.

Amefahamisha kwamba mfumo rasmi ulioweka mawaziri ulikuja mwaka 1960 na kukatolewa muongozo na sheria za jumla za utumishi ulioweka wajibu, kwa viongozi mbali mbali wakiwemo watumishi , viongozi mawaziri na wakurugenzi sambamba na kuwepo Kamisheni ya Utumishi wa umma kusimamia utumishi wa kiserikali.

Mhe. Makamu amewataka watumishi wa umma Zanzibar kufanya kazi kwa kuzingatia wujibu ,  taratibu  na kanuni za kiutumishi za leo ambazo unakwenda na mfumo wa Kikatiba katika kuchangia maendeleo ya nchi kwa haraka.

Amesama licha ya utumishi wa umma Zanzibar kupita katika vipindi vingina hatua mbali mbali ni vyema sasa kuelekeza utumishi  huo kulingana na katiba sheria na katuni za nchi  kwa kuwa ndio vinavyoongoza utumishi huo sambamba na kuzingatia utamaduni wa sasa wa kuendesha nchi.

Amesema kwamba Zanzibar kwenye utumishi wa umma umepita katika  vipindi tofauti  na kwamba sasa jambo muhim u ni kuwepo mfumo wa kikatiba wa utumishi  na kwamba dunia ya sasa inazingatia ushindani katika kuendesha nchi na kwamba ukiwa na serikali isiyokuwa na ufanisi huwezi kupata maendeleo na kuwataka watumishi na viongozi kuzingatia hilo ili taifa liweze kusonga mbele .

Amewataka watumishi na viongozi kuhakikisha kwamba wanafuata maadili kutokana na umuhimu wake hasa katika utoaji wa huduma kwa uaminifu mkubwa wa kimaadili.

Amesema kwamba watu wanotumikiwa wanaawaminisana  viongozi kutokana na imani ya kuwepo maadili mema waliyonayo watumishi na kwamba yasipozingatiwa uaminifu na imani kwa wanaotumikiwa itapotea.

Amesama kwamba upo uhusuinano mkubwa baina ya maadili  na kumtengeneza mazingira ya kuamini katika kazi tunazofanya na kujengea imani  wanaoutumikiwa ambao ni wananchi na kwamba ni jambo la muhimu sasa kushikamana na maadili.

Amewataka  viongozi wote kuzingatia sana uwezo , tabia na mwendendo mwema binafsi wa mtumishi  tangu wakati ajira  yake kwa kuwa wanaoajiriwa bila kuwa na maadili tokea awali sio rahisi kuwa na kuzingatia maadili katika mahala pa kazi.

Amewataka watumishi na viongozi kuachana na imani zao za siasa wakati wa utekelezaji wa majukumu yao mbali mbali ya kiutumishi  kwa kuwa bila kufanya hivyo ufanisi  wa kazi hautopatikana.

Amesema kwamba kuchanganya imani za kisiasa katika utumishi wa umma ni dhambi kubwa ambayo inaweza kuharifu mfumo na maendeleo ya kazi huku kukuwepo idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji kuhudumiwa hawana ufuasi wa vyama .

 Amewataka watumishi kuacha  kuchanganya siasa za vyama na kwamba hapa Zanzibar hali hiyo imechangia sana kuharibu utumishi wa umma na kwamba ni wajibu wa viongozi na watumishi warudi kwenye mstari  kwa kutotumia imani za siasa katika kutekeleza majukumu yao.

Aidha amewataka viongozi kufahamu kwamba ni walizi wa haki za watumishi wote na kwamba hata iwapo mtumishi haijui haki yake kiongozi anawajibu wa kuhakikisha kwamba haki hiyo imepatikana kwa kudaiwa ama hata kwa kutodaiwa na mtumishi mwenyewe.

Naye waziri wa nchi  ofisi ya Makamu wa Kwanza wa rais Mhe. Harous Said Suleiman, amesema kwamba mafunzo hayo ni katika fursa muhimu kwa watendaji na wafanyakazi nchi  katika utoaji wa huduma na kujenga ufanisi katika kuutumikia umma.

Kwa upande wake  Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dk. Omar Dad Shajak amesema kwamba mafunzo hayo yanalenga kutekeleza kwa vitendo agizo la serikali la kuhakikisha kwamba watumishi wote wa umma wanapatiwa taaluma  juu ya sheria, maadilini na usalama kazini.

 Imetolewa na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha habari leo tarehe 15.04.03

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.