Habari za Punde

WHO YATOA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA MAAFA

Na Rahma Khamis,Melezo                    24.04.2023

Katibu Mkuu Ofisi   ya Makamo wa pili wa Rais  Islam Seif Salim ameliomba Shirika la Afya Duniani WHO kuendelea kuisadia Zanzibar katika kukabiliana na maafa pindi yanapojitikeza.

Ameyasema hayo katika Hoteli ya Visitor Inn Jambiani wakati alipokua akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wa Taasisi mbalimbali juu ya  kukabiliana na maafa.

Amesema Serikali inatambua mchango unaotolewa na Shirika hilo katika sekta mbalimbali hivyo ameliomba Shirika hilo kuendelea kuongeza nguvu  ya kusaidia  hasa katika kukabiliana na majanga yanayojitokeza ambayo huathiri jamii na Taifa kwa ujumla.

Aidha amefahamisha kuwa lengo la  mafunzo hayo ni kuhakikisha nchi za kiafrika zinaweza kutumia rasilimali walizonazo katika kukabiliana na maafa pindi yanapojitokeza.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yatawasaidia watendaji kuweza kukabiliana na maafa yanayoendelea kuathiri  afya za watu ,miundombinu na mazingira siku hadi siku
"wakati yanapotokea maafa mambo mbaalimbali hujitokeza kama maradhi ya mripuko,watu kukosa makaazi na hata miundo mbinu kuharibika,hivyo mafunzo haya yatawawezesha waatendaji kuweza kukabiliana nayo wakati wowote yanapotokea" Katibu alisema.

Hata hivyo Katibu huyo  aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kua na umoja   na kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili jamii iwe salama.

Nae Mwakilishi Mkaazi wa  Shirika la Afya Duniani (WHO) Zanzibar Dkt. Andermichael Gihrmy amewataka washiriki  wa mafunzo hayo kuwa makini na kushiriki ipasavyo katika mafunzo hayo  ili kuweza kufikia lengo  lililokusudiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Utumishi Wizara ya Afya  Mwatoum Ramadhan Mussa amewata washiriki kuwa wasikivu na watulivu wanaopatiwa mafunzo hayo ili kuitumia vyema fursa hiyo itakayosaidia kuweza kukabiliana na maafa yanapotokezea Nchini .

Mafunzo hayo ya siku 24  yameandaliwa na Shirika la Afya Duniani WHO  ambapo yameshirikisha watendaji kutoka Taasisi mbalimbali ikiwemo Kilimo, Afya, Mazingira, Maji, Ustawi waJamii na Maafa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.