Habari za Punde

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Hamis Mwinjuma Akonga Mashabiki katika Tamasha la Bongo Flavour Honours

 


Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma Mei 26, 2023  katika Ukumbi wa Alliance Francaise Jijini Dar es Salaam ameshiriki Tamasha la Muziki la  Bongo Flavor Honors lenye lengo la kutoa heshima kwa wakongwe wa muziki huo.

Mhe. Mwinjuma ameungana na wasanii wa muziki huo akiwemo Msanii JayMoe  kutoa burudani kwa mashabiki waliokuepo.

Wasanii wengine walitoa burudani ni Msanii Sugu, Mchizi Mox, Dully Sykes na wengine.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.