Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na mgeni wake Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Mhe.Michael Mattle,alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.
SERIKALI ya Mapinduzi
ya Zanzibar imesema imeweka kipaumbele zaidi kuimaisha miundombinu ikiwemo
barabara safi zenye kiwango cha lami kwa mji miji yote ya Zanzibar ili
kurahisisha sekta ya biashara na kuwavutia wawekezaji zaidi nchini.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo Ikulu,
Zanzibar alipozungumza na Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Michael Battle,
aliefika kujitambulisha.
Dk. Mwinyi, pia
ameikaribisha Marekani kuangalia fursa za biashara na uwekezaji katika
kuimarisha uhusiano wao mwema utakaofungua milango ya fursa nyinyi za ajira kwa
wananchi wa Zanzibar.
Akizungumzia sera ya
Uchumi wa Buluu, Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi Battle kwamba Zanzibar
imejaaliwa bahari nyenye fursa nyingi za uwekezaji na biashara kupitia sekta ya
utalii endelevu, uvuvi pamoja kilimo cha mwani.
Alisema sekta ya
Uchumi wa buluu pia ina fursa za utalii wa ufukweni, utalii wa michezo ambako
pia aliikaribisha Marekani kuangalia maeneo hayo kwaajili ya uwekezaji na
kuimarisha uhusiano wao utakaolenga kukuza uchumi kwa watu wa pande mbili hizo.
Alisema, uhisusiano
wa diplomasia baina ya Tanzania na Marekani ni wa muda mrefu pia alieleza
Zanzibar ikiwa sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, imefaidika na
uhusiano huo hasa kupitia sekta za Afya na Elimu.
Akizungumza kwenye
hafla hiyo, Balozi Michael Battle ameisifu Zanzibar kwa kubarikiwa visiwa
vyenye rasilimali nyingi za Uchumi.
Balozi Battle
alimueleza Rais Dk. Mwinyi, dhamira ya Marekani kuwekeza kwenye biashara kwani
wanajivunia kuwa na raia wengi, Tanzania.
Pia, alisema fursa ya
kuwekeza Zanzibar, itafungua ajira nyingi kwa Wazanzibari na Wamareakani
waliopo, kuongeza mitaji na kuboresha ustawi wa watu wa Tanzania na Marekani
waliopo Zanzibar.
Hata hivyo, Balozi
Battle alitumia fursa hiyo, kuipongeza Tanzania kwa kutimiza miaka 59 ya
Muungano baina ya Zanzibar na Tanganyika, alisifu ni Muungano wa Mfano kwa
dunia ya sasa.
Uhusiano wa
Diplomasia baina ya Tanzania na Marekani ulianza zaidi ya miaka 50 iliyopita
kwa mataifa mawili hayo kushirikina kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo,
jamii na uchumi.
Tanzania ina ubalozi wake nchini Marekani kwenye mji mkuu wa nchini hiyo, Washington DC, ambapo Balozi, Elsie Sia Kanza ni Balozi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania anaeiwakilisha Tanzania kwa Marekani na Mexico.
Marekani iko
Kaskazini mwa bara Amerika, inapakana na nchi ya Canada kwa upande wa Kaskazini
na Kusini ipo jirani na Mexico.
Taifa la Marekani
lina idadi ya watu milioni 333, ni nchi ya tatu kwa ukubwa duniani,
inashirikiana mipaka ya bahari na visiwa vya Bahamas, Cuba, nchi ya Urusi na
mataifa mengine. New York ni jiji kubwa la biashara nchini humo.
IDARA YA MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment