Mkoa wa Kusini Unguja,
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT- Wazalendo Zanzibar Mhe, Mhe. Othman
Masoud Othman, amesema kwamba rasilimali za nchi zilizopo ni mali ya wananchi
na kwamba kila kiongozi mwenye dhamana anawajibika kuzisimamia kwa uwazi, uaminifu
na uadilifu ili kuleta maendeleo kwa niaba ya wananchi wenyewe.
Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar, ameyasema hayo huko
Chwaka Wilaya ya Kati Unguja, alipohutubia wananchi na wafuasi wa Chama
hicho katika mkutano wa hadhara akielekea
kukamilisha mfululizo wa mikutano ya aina hiyo katika wilaya zote za Unguja na
Pemba tokea kuruhusiwa kwa mikutano ya kisiasa nchini Tanzania.
Mhe Makamu amefahamisha kwamba nchi
zote duniani zilizoweza kupiga hatua
hazikuwa na miujiza bali imetokana na viongozi wao kuwa waadilifu , waamini na
wanaowajibika vyema kwa wananchi sambamba
kuwa na uwezo mkubwa wa kupanga na kujiamulia wenyewe mambo ya nayohusu
maendeleo yao.
Aidha Mhe. Othman mesema kwamba ili
Zanzibar iweze kuendelea na kupiga hatua
katika nyanja mbali mbali za kiuchumi na maendeleo inahitaji uwajibikaji
na uadilifu kwa viongozi wanaoshika nafasi mbali mbali ili kuweza kuleta maendeleo
ya wanachi katika sekta na nyanja tofauti.
Amefahamisha kwamba ahadi ya chama
hicho kwa wananchi wa Zanzibar ni kupigania jitihada za maendeleo kwa pamoja na
kwa kuweka misingi imara zaidi ya uwajibikaji wa viongozi wanaoshika dhamana
mbali mbali za kuwatumikia wananchi na pale wanaposhindwa kutekeleza majukumu
yao ipasavyo viongozi hao waweze kuwajibishwa na wananchi wenyewe.
Amesema kwamba siri ya mafanikio ya
kimaendeleo katika taifa ,lolote duniani ni kuendesha na kusimamia masuala ya
nchi kwa misingi ya uwazi na kuwepo viongozi wanaopewa dhamana wenye uwezo
mkubwa waa kutekeleza na pia kusimamia vyema majukumu yao waliyopewa .
Aidha amesema kwamba kazi moja ya
chama cha siasa ni kuhakikisha kwamba wanawasimamia ipasavyo viongozi na
serikali kwa jumla na kuwasemea wananchi
hasa kwa vile chama na serikali ni vitu viwili tafauti katika kuisimamia
serikali ili kujenga taifa imara lenye viongozi wenye nidhamu na uwajibikani na
pia kuepuka kufanya ufisadi.
Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama
hicho ambaye pia ni Waziri wa Biashara
na Mandeleo ya Viwanda Zanzibar Mhe. Omar Said Shaaban, amesema kwamba ahadi ya
chama hicho kwa wazanzibari ni kuwaletea
wanchi pamoja katika Zanzibar yenye umoja katika jitihada za kuijenga nchi yao.
Aidha amesema kwamba chama hicho kitaendelea kuwa cha kusimamia
haki, umoja na mishakamano
kwa wanyonge na kujenga taifa lenye
maadili ya wazanzibari kwa kuwa hiyo
ndio moja wapo ya kazi ya chama cha Siasa .
Mwisho
Kitengo cha Habari
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar
30, Julai, 2023
No comments:
Post a Comment