Habari za Punde

Mhe Othman akutana na Rais wa shirika la Kimataifa linalojishughulisha na kuwezesha maendeleo endelevu kwa jamii (PACT)


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman  akimsikiliza Rais wa shirika la Kimataifa linalojishughulisha na kuwezesha maendeleo endelevu kwa jamii (PACT) Dk. Caroline Anstey, lenye makao makuu yake nchini Marekani.  Ujumbe huo ulifika ofisini kwa makamu Migombani mjini Zanzibar leo tarehe 24.08. 2023 kwa kubadilishana mawazo na Mheshimiwa Makamu . ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.)

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman  akizungunza na ujumbe  wa shirika la Kimataifa linalojishughulisha na kuwezesha maendeleo endeleovu kwa jamii (PACT) lenye makao makuu yake nchini Marekani.  Ujumbe huo ulifika ofisini kwa makamu Migombani mjini Zanzibar leo tarehe 24.08. 2023 kwa kubadilishana mawazo na Mheshimiwa Makamu . 

( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.)



Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba  suala la ukosefu wa ajira kwa vijana wa Zanzibar linalendelea kuwa changamoto kubwa inayohitaji jitihada za  pamoja kwa mashirikiano kati  serikali na  Wadau mbali mbali wa maendeleo katika kuandaa sera na mipango sahihi na kuweka mikakati madhubuti ya utekelezaji katika  kulikabili  kwa ufanisi suala hilo.

Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipofanya mazungunzo na Shirika la Kimataifa lisilo la Serikali (PACT) , ambalo kwa kushirikiana na serikali mbali mbali duniani linajishughulisha kuwezesha maendeleo endelevu kwa jamii, uimarishaji wa Utawala bora na Demokrasia, na kuhudumia watu wenye changamoto  na kuleta afua katika sekta za lishe ,elimu , uwezeshaji kiuchumi na utafutaji wa masoko.

Mhe. Makamu amesema kwamba tatizo hilo ni kubwa  na limekuwa kuongezeka kwa kasi kila mwaka kwa kuwa vijana wengi wanaendelea kukosa ajira na hivyo kuashiria kwamba jambao hilo linaweza kugeuka kwa ni janga la baadae katika nchi jambo ambalo linahitaji jitihada kubwa katika kuwawezesha vijana kwa kutumia rasilimali za ndani zilizopo hasa katika sekta ya utalii.

Amefahamisha kwamba Zanzibar hivi sasa ina hoteli za utalii zaidi mia sita, lakini mahitaji makubwa ya hoteli hizo yanapatikana kutoka nje ya Zanzibar, na iwapo vijana  nchini watawezeshwa ipasavyo sekta hiyo pekee inaweza kuwa na uwezo na kutoa fursa kubwa za kutatua tatizo la ajira kwa vijana nchini.

Aidha Mhe. Othman amesema kwamba kupitia juhudi za pamoja kati ya serikali na Taasisi zisizo za Serikali kama vile PACT inawezekana kuwawezesha vijana kujengewa uwezo wa kujiajiri katika uzalishaji wa bidhaa mbali mbali zinazohitajika katika soko la utalii  jambo ambalo litasaidia sana katika kuikabili changamoto ya ukosefu wa ajira nchini.

Amefahamisha kwamba serikali haina uwezo wa kuwaajiri vijana wote waliopo na wanaomaliza katika vyuo vikuu mbali mbali lakini kinachohitajika ni kuwepo mazingira sahihi ya kuwawezesha katika sekta ya biashara ya utalii na ukarimu na kwamba bila kuwawezesha vijana katika ajira taifa haliwezi kuwa na mabadiliko chanya kimaendeleo.

Mhe. Othman amesema  kwamba vijana katika taifa lolote wanapaswa kuandaliwa kuwa chachu ya mabadiliko ya kimaendeleo  kwa kuangalia mahitaji yao muhimu kwa sekta na maeneo tofauti kwa kuzingatia mahitaji ya  wakati wa sasa na wabaadae ili taifa liweze kupiga hatua Zaidi na kwa haraka.

Akizungunzia suala la athari zinazotokana na mabadiliko ya tabia nchi Mhe. Makamu amesema kwamba Zanzibar kuna maeneo yapatayo kumi na nne (14), yamekumbwa na athari hiyo ingawa juhudi kubwa zimekuwa zikichukuliwa na serikali ikiwa ni pamoja na upandaji wa mikoko lakini tatizo la athari hizo bado linaendea  katika maeneo mbali mbali nchini.

Hata hivyo, amesema kwamba serikali inaendelea na mikakati mbali ya kitaifa na kwamba hivi karibuni itazindua mradi  wa kuirejesha Zanzibar kuwa ya kijani ambapo utekelezaji wake utahitaji ushiriki wa wadau mbali mbali wa maendeleo katika kufikia ufanisi wa lengo lililokusudiwa la kupunguza athari za  mabadiliko ya taibia nchi.  

Akizungunzia suala la  vijana katika siasa Mhe. Othman amesema kwamba wengi wao wanaingia katika siasa kwa matumaini ya kupata ajira badala ya kufikiria kuwepo mabadiliko ya kimaendeleo jambo ambalo linabakia kuwa ni changamoto kuwa kwa vijana.

Naye Rais wa shirika hilo la PACT Dk. Caroline Anstey, amesema kwamba shirika hilo limekuwa likifanya kazi kubwa na jamii katika nchi mbali mbali duniani katika kuweka ustawi wa masuala ya afya kwa jamii pamoja na kusaidia kujenga uwelewa kwa vijana katika masuala mbali mbali ikiwemo demokrasia, elimu na utawala bora.

Amesema kwamba shirika hilo lenye makao yake makuu nchini Marekani lipo tayari kufanya kazi na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika maeneo mbali mbali ya kuwawezesha vijana katika masuala, elimu , afya, ustawi wa jamii na demokrsia pamoja na utawala bora na hivi sasa wanafanyakazi katika nchi 35 duniani kote.

Mwisho

 

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais  wa Zanzibar

Agosti 24, 2023




 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.