Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Azungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan Tanzania

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Viongozi wa Kanisa la Anglikan Tanzania ukiongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan Tanzania Maimbo Mndolwa (kulia kwa Rais) mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo,30-8-2023.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imekua ikihamasisha na kushajihisha watu wake kujitahidi kuzitumia vema fursa za lugha ya Kiswahili na kuzifanyia kazi ya kutafsiri kwenye mataifa mbalimbali duniani.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amehyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Maimbo Mndolwa aliefika kujitambulisha na ujumbe wake baada ya kuchaguliwa kuongoza kanisa hilo mwezi Februari mwaka huu, kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Dk. Mwinyi alisema lugha ya Kiswahili imekua na fursa nyingi duniani kutokana na kazi za ukalimali, hivyo aliwataka Wazanzibar na Watanzania kwa ujumla kutumia fursa hizo kwa kuzichangamkia kwa wingi na kuahidi ushirikiano baina ya kanisa na Serikali kuwashajihisha vijana kuzichangamkia

“Sasa hivi tunapromote sana watu wetu kwenda kufanyakazi za kutafsiri lugha ya Kiswahili, lakini wenzetu mataifa mengine wametuzidi, tunakazi ya kufamuya tuko tayari kushirikiani na nyinyi kwaajili ya vijana wetu” alieleza Rais Dk. Mwinyi.

Aidha, rais Dk. Mwinyi alimuahidi askofu huyo kuzungumza na wahusika wa kamisheni ya Kiswahili ili kuona namna ya kuboresha ushirikiano baina ya serikali na kanisa hilo.

Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekua na uhusiano wa muda mrefu na kanisa hilo, hivyo aliutaka uongozi huo mpya kuendeleza ushirikiano wao kwa Serikali hasa kwenye suala zima la kuendelea kuhubiri amani, umoja na mshikamano kwani ni                     mambo muhimu kwa usatawi na ujenzi wa Serikali na watu wake.

Akizungumzia masuala ya kuboresha Utalii Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alilipongeza Kanisa La Anglikana kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwavutia watalii wengi sambamba na kupongeza hatua ya Kanisa hilo kuwaalika watu wa kubwa duniani kuja Zanzibar hali itakayozidi kuitangaza Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kimataifa pamoja na kukuza sekta ya utalii.

Pia, Rais Dk. Mwinyi alilipongeza Kanisa hilo kwa juhudi zao za kupinga harakati za biashara ya kuuza binaadamu ambayo imeshamiri sana duniani sambamba na kumueleza Askofu Maiombo kwamba Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar inaungamkono hatua hiyo, wadau na wanaharakati wote wanaopinga udhalimu huo.

Rais Dk. Mwinyi aliupongeza na kuukariribisha uongozi wa Kanisa hilo na kuueleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekua na ushirikiano mzuri na kanisa hilo hivyo aliomba kuendeleza uhusiano uliopo kwa manufaa ya wanaumini wao na Serikali kwa ujumla

Naye Askofu Maimbo Mndolwa alimpongeza Rais wa Zanzibar kwa maendeleo makubwa aliyoyafanikisha kipindi kifupi cha uongozi wake.

Askofu Maimbo alimueleza Rais Dk. Mwinyi mpango wa Kanisa hilo kutumia historia ya biashara ya utumwa Zanzibar, kama ni fursa adhimu ya kukuza utalii kwa Zanzibar kupitia kanisa hilo ambalo limekua kivutio kikubwa kwa watalii wengi wanaofika nchini.

Alimuahidi Rais Dk. Mwinyi kwamba kanisa linampamgpo wa kuwaalika mataifa makubwa akiwemo Gavana mkuu wa Ujerumani kuja Zanzibar kwani taifa hilo liliacha athari na histotia kubwa ya biashara ya utumwa Zanzibar pamoja na mataifa mengine ya Mashariki ya mbali kwa lengo la kuitangaza Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwa njia za utalii pia kuweka mkazo kwenye sekta hiyo.

Sambamba na kuishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuangalia uwezekano wa kuimarisha kiiutalii maendeneo ya kanisa hilo kwani limekua kivutia kikubwa kwa wageni na kuiomba Serikali kuangalia namna ya kufunga mashine za kudhibiti mapato yanayotokana na utalii ili kuzuia mianya ya kodi za Serikali zisipotee mikononi mwa wasiohusika.

Akizungumzia umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwenye anga za Kimataifa Askofu Maimbo alimomba Rais Dk. Mwinyi ushirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Kamisheni ya Kiswahili kushirikiana kuwaandaa vijana ili wakawe wakalimali wazuri kimataifa kwani nafasi nyingi nimechukuliwana Wakenya na Wakongo.

Alieleza Tanzania ina fasaha nzuri ya lugha ya kiswahilli hivyo aliziomba Serikali za SMZ na SMT kwa ushirikkiano wa Kanisa la Anglikana Tanzania kuitumia fursa hiyo kwa watanzania kunufaika.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Viongozi wa Kanisa la Anglikan Tanzania ukiongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan Tanzania Maimbo Mndolwa (kulia kwa Rais) mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo,30-8-2023.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Viongozi wa Kanisa la Anglikan Tanzania ukiongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan Tanzania Maimbo Mndolwa (kulia kwa Rais) mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo,30-8-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan Tanzania Askofi Maimbo Mndolwa, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 30-8-2023, kwa mazungumzo na kujitambulisha.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mgeni wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikan Tanzania Askofu Maimbo Mndolwa, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 30-8-2023, alipofika kwa mazungumzo na kujitambulisha.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.