Habari za Punde

Hafla ya kuagwa Madaktari wa Kichina Ikulu

Viongozi wa Wizara ya Afya na Hospitali ya Mnazi Mmoja wakiwa katika hafla ya kuagwa Madaktari wa Kichini waliokuwa wakitoa huduma katika Hospitali za Zanzibar waliofika Ikulu Jijini Zanzibar Kuagana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi leo.
Baadhi ya Madaktari wa kichina na Mkalimani wakifuatilia kwa makini sherehe ya Kuagwa kwao waliofika Ikulu Jijini Zanzibar leo Kuagana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akimsikiliza Kiongozi wa  Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun (kulia aliyesimama) wakati akitoa shukurani zake leo kwa Ushirikiano walioupata katika  huduma walizozitoa katika Hospitali za Zanzibar,wakati hafla ya kuagana wa lipofika Ikulu Jijini Zanzibar.
Viongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina wamsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa hutuba yake wakati walipofika kumuaga Rais leo Ikulu Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari wa Kichina 32 waliuomaliza muda ambao wakitoa huduma katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,mazungumzo yalifanyika leo walipofika  Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya China kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.

Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alipowakabidhi vyeti na medali timu ya madaktari 32 kutoka China waliohudumu kwenye hospitali za Zanzibar kwa kipindi cha mwaka mmoja na kuwaaga baada ya kumaliza muda wao nchini.

Rais Dk. Mwinyi amesema, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi kutoka China kupitia sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo Afya hususan kupokea timu za madaktari bingwa wanaofika nchini kubadilishana uzoefu na wazawa hali aliyoieleza imeimarisha uhusiano mwema uliopo baina yao pamoja na kujifunza uzoefu wa masuala mbalimbali ya afya.

Dk. Mwinyi alieleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendeleza maeneo mengi ya afya kwa kujenga hospitali zenye vifaa tiba vya kisasa, kuboresha miundombinu na kuongeza hospitali za wilaya na mikoa pamoja na kuifanyia matenegezo makubwa hospitali ya Mnazi Mmoja.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameshukuru kazi kubwa iliyofanywa na timu hiyo ya madaktari 32 kipindi chote walichohudumu Zanzibar na kusema Serikali ilnajivunia sana kuwepo kwao.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Waziri wa Afya Nassor Ahmed Mazrui alisema aliishukuru timu ya madaktari hao nakueleza ushirikiano uliopo baina ya China na Zanzibar umedumu kwa miaka 60 sasa.

Naye, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk. Amour Suleiman Mohammed alisema timu hiyo ya madaktari bingwa kutoka China iliwasili nchini Septemba 26 mwaka 2022 na Septemba 26 mwaka huu inatarajiwa kurejea kwao.

Alisema timu hiyo ilitoa msaada wa kitabibu kwa wananchi wa Unguja na Pemba kwa magonjwa ya macho, meno, mkojo, figo, huduma za X- ray, pia ilifanya upasuaji  kwa wagonjwa zaidi ya 50 kwa maradhi tofauti.

Kiongozi mkuu wa timu ya madaktari hao 32 , Dk. Zhao Xiaojun alishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano ilioutoa kipindi chote na kueleza Zanzibar ni visiwa vyenye upendo, amani na mshikamano kwa wenyeji  na wageni.  

Alishukuru pia ushirikianao kwa wenyeji wao madaktari wa Zanziba na kueleza upendo wao ulikakisi maudhui ya uwepo wao nchini

“Kamwe hatutasahau uzuri na haiba ya mandhari ya visiwa vya Zanzibar vilivyopambwa kwa maumbile ya anga la buluu, fukwe nyeupe, uzuri wa mwanga wajua linapochomoza, kijani cha minazi na ukarimu wa watu wake, yote haya tutayakosa baada ya kuondoka Zanzibar” kwa hisia alisifia

Hata hivyo, timu ya madaktari hao ilimuahidi Dk. Mwinyi kuendeleza ushirikiano uliopo baina yao.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari wa Kichina 32 waliuomaliza muda ambao wakitoa huduma katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,mazungumzo yalifanyika leo walipofika  Ikulu Jijini Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akimkabidhi zawadi  Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun   wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari hao wa  Kichina  32 waliomaliza muda   wao wakutoa huduma  mbali mbali  katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,hafla ya kuagana ilifanyika leo  ukumbi wa  Ikulu Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akipokea  zawadi  kutoka kwa Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun   wakati wa kuagana na  Ujumbe hguo wa Madaktari 32 waliomaliza muda  wa kutoa  huduma  mbali mbali  katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,katika hafla  iliyofanyika leo  ukumbi wa  Ikulu Jijini Zanzibar.
 [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.