Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi ashiriki Sala ya Ijumaa pamoja na Maulidi ya Mtume Kidombo

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dkt.Salmin Amour Juma. Ndg.Amini Salmini Amour, alipowasili katika viwanja vya Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa ajili ya kuhudhuria Ibada ya Sala ya Ijumaa na kuhudhuria shughuli ya Maulid ya Mfungo Sita ya Kidombo na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee, iliyofanyika baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa leo 6-10-2023. na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, wakiwa katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja, kwa ajili ya Ibada ya Sala ya Ijumaa na kuhudhuria Maulidi ya Mfungo Sita ya Kidombo na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee, iliyofanyika baada ya kumaliza kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika msikiti huo leo 6-10-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi wa Kijiji cha Kidombo katika kisomo cha hitma na dua ya kuwaombea Wazee, baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo, na kuhudhuria Maulidi ya Mfungo Sita hufanyika kila mwaka Kijijini hapo na (kulia kwa Rais) Ndg. Amini Salmini Amour na (kushoto kwa Rais) Mzee wa Kijiji cha Kidombo Sheikh.Salum Juma, wakisoma hitma 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi wa Kijij cha Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja katika kisomo cha Hitma na dua ya kuwaombea Wazee wa Kidombo, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo leo 6-10-2023, na (kulia kwa Rais) Mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dk.Salmini Amour Juma Ndg.Amini Salimini Amour.Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman na (kushoto kwa Rais) Mzee wa Kijiji cha Kidombo Sheikh. Salum Juma,Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi, Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.
Waumini mbali mbali wakiwa katika kisomo cha Khitma na Dua maalum sambamba na  Maulid ya Mtume Muhammad (SAW) yaliyofanyika leo katika Msikiti wa Ijumaa Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja,yaliyohudhuriwa na Viongozi mbali mbali wa Kitaifa akiwa Mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi(hayupo pichani).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi wa Kijiji cha Kidombo, akiitikia dua ya kuhitimisha hitma ya kuwaombea Wazee wa Kijiji cha Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja ikisomwa na Sheikh. Salum Juma (kushoto kwa Rais) na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi na (kulia kwa Rais) Ndg. Amini Salmini Amour na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Othman, iliyofanyika katika Msikiti wa Mkuu wa Ijumaa Kidombo leo 6-10-2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiongozana na Viongozi wa Serikali wakielekea nyumbani kwa Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dk.Salmini Amour Juma kwa ajili ya kumsalimia baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee wa Kijiji cha Kidombo, iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja leo 6-10-2023, (kushoto kwa Rais) Ndg. Amini Salmini Amour na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mohmoud na (kulia kwa Rais) Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Othman na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla
RAIS Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dk.Salmini Amour Juma akijumuika na Viongozi wakuu wa Serikali katika kuitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi (hayupo pichani) walipofika nyumbani kwake Kidombo kwa ajili ya kumsalimia baada ya kumalizika kwa kisomo cha hitma na dua ya kuwaombea Wazee iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja leo 6-10-2023, na (kulia kwa Alhajj Salmini) Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmuod na (kushoto kwa Alhajj Salmini ) Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman na Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein
RAIS wa Zanzibar na Mwemyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Wananchi wa Kijiji cha Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja leo 6-10-2023, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee wa wa Kidombo, iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo.
WANANCHI wa Kijiji cha Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja wakimsalimia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi, wakati akiwasalimia baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee wa Kidombo, iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja leo 6-10-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia Watoto wa Kijiji cha Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja,baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee wa Kijiji hicho iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo leo 6-10-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Watoto wa Kijiji cha Kidombo Mkoa wa Kaskazini Unguja, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee wa Kijiji hicho iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo leo 6-10-2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na kisomo cha Hitma na Dua ya kuwaombea Wazee wa Kijiji Kidombo iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Kidombo leo 6-10-2023.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi amejumuika na waumini wa Kiislamu kwenye Ibada ya Sala ya Ijumaa, huko Mkwajuni Kidombo, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Mbali na ibada hiyo, Alhaj Dk. Mwinyi pia ameshiriki kwenye hitma na du’a maalum zilizosomwa baada ya ibada ya Sala ya Ijumaa kwa kuwaombea viongozi waliopo serikalini, wastaafu, masheikh na wazee walio hai na waliofariki dunia, ndani na nje ya Kijiji hicho.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali akiwemo Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Marais wastaafu, Alhaj Dk. Salmini Amour Juma na Alhaj Dk. Ali Muhamed Shein, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh, Saleh Omar Kaab, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ayoub Mahmoud na viongozi wengine wa dini.

Alhaj Dk. Mwinyi pia alipata wasaa wa kusalimiana na wananchi wa Mkoa huo wa Kaskazini Unguja na kuwatakia kheir.

Akikhutubu kabla ya sala ya Ijumaa Khatib Sheikh, Abdulkarim Said Abdulla kutoka Ofisi ya Mufti wa Zanzibar, aliwasihi wananchi kuendelea kuwaombea du’a njema viongozi wa Serikali kwa kazi kubwa wanazozifanya za kuitumikia nchi na harakati zao za kuendelea kuiletea maendeleo.

Pia aliwaomba viongozi hao kuwaomba viongozi hao kuendelea kuwatumikia, kuwapenda na kuwahurumia raia.

Pia, Sheikh Abdulkarim aliikumbusha jamii ya Kiislam juu ya suala zima la kumpenda Mtume Muhammad (SAW) kwa kufuata mema yote na kuachana na mabaya aliyoyakataza

Ibada hizo zilitekelezwa kufuaftia mwaliko kwa viongozi wa Kitaifa unaotolewa kila mwaka na Rais Mstaafu, Alhaj Dk. Salmin Amour Juma, ulioambatana na sherehe za usomwaji wa Maulid ya kumswalia Mtume Muhammad (SAW), kiijijini hapo.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.