Habari za Punde

Waziri Mkuu Mhe.Majaliwa Atoa Agizo Wasimamizi wa Mji wa Serukali

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wasimamizi na wataalamu wa ujenzi wa Mji wa Serikali jijini Dodoma wahakikishe matarajio ya ujenzi huo yanafikiwa kama ilivyokusudiwa.

 

Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea Kusini, Mheshimiwa HyeongRyeol Kim.

 

Amekutana na kiongozi huyo leo Ijumaa, Januari 26, katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni Jijini Dar es Salaam, baada ya hafla ya utiaji saini mikataba ya makubaliano kati ya taasisi za Korea Kusini na Tanzania.

 

Makubaliano hayo yanahusu kubadilishana uzoefu juu ya usimamizi na uratibu wa uendelezaji wa makao makuu na mji wa Serikali pamoja masuala ya ujenzi vikiwemo viwanda, hoteli.

 

Utiwaji saini huo umefanyika kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi Uendelezaji wa Mji wa Segong na kampuni ya Heerim ya Korea Kusini katika masuala ya usanifu na ubunifu wa ujenzi kwenye Mji wa Serikali na Makao Makuu jijini Dodoma.

 

“Serikali ya Tanzania na Korea Kusini zina mahusiano mazuri ya kidiplomasia, hivyo matarajio yetu ni kuona Makao Makuu na Mji wa Serikali jijini Dodoma unakuwa mzuri.”

 

Kwa upande wake, Mheshimiwa HyeongRyeol Kim amesema utiaji saini wa makubaliano hayo ni fursa muhimu ya kuendeleza ushirikiano baina ya mataifa hayo.

 

Pia, Mheshimiwa Kim amemshukuru Waziri Mkuu kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na amemuhakikishia kwamba nchi yao itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuliendeleza jiji la Dodoma.

 

 (mwisho)

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

IJUMAA, JANUARI 26, 2024.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.