Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe Dkt. Philip Mpango akishiriki Kongamano la
Kimataifa la Dhima ya Lugha za Asili katika kuendeleza Diplomasia ya Kiuchumi
na Kiutamaduni lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Four Points by
Sheraton Jijini Dar es salaam tarehe 20 Februari 2024. Kushoto ni Rais Mstaafu
wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Joackim Chissano na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya
Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe Dkt. Philip Mpango akipokea Tuzo ya Amani
Duniani iliyotolewa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia
Suluhu Hassan wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Dhima ya Lugha za
Asili katika kuendeleza Diplomasia ya Kiuchumi na Kiutamaduni lililofanyika
katika Ukumbi wa Mikutano wa Four Points by Sheraton Jijini Dar es salaam
tarehe 20 Februari 2024. Tuzo hiyo imetolewa na Chuo kikuu cha Dar es salaam
kupitia Kigoda cha Uprofesa cha Mwl. Julius Nyerere katika Kiswahili.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe Dkt. Philip Mpango akizungumza na Rais
Mstaafu wa Jamhuri ya Msumbiji ambaye ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wakuu wa Nchi na Serikali
Wastaafu katika Afrika Mhe. Joachim Chissano wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Dhima ya Lugha za Asili katika kuendeleza
Diplomasia ya Kiuchumi na Kiutamaduni lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano
wa Four Points by Sheraton Jijini Dar es salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Philip Mpango akiwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Joackim Chissano, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolph Mkenda, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kwazulu Natal cha Afrika Kusini Prof. Nhlanha Mkhize katika picha ya pamoja na washiriki mbalimbali wa Kongamano la Kimataifa la Dhima ya Lugha za Asili katika kuendeleza Diplomasia ya Kiuchumi na Kiutamaduni lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Four Points by Sheraton Jijini Dar es salaam tarehe 20 Februari 2024.
No comments:
Post a Comment