Na.Mwandisi OMWR.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba ziara za kuwatembelea
waananchi wenye matatizo mbali mbali katika maeneo wanayoishi ni muhimu kwani
ni fursa kubwa kwa viongozi katika ngazi tofauti kujifunza na kujua hali halisi
ya maisha yao waliyonayo.
Mhe. Othman ambaye pia ni Mwenyekiti
wa Chama cha ACT – Taifa ameyasema hayo mkoa
wa Kaskazini Unguja akiwa katika muendelezo wa ziara ya kuendeleza utamaduni wa
kuwatembelea wagonjwa, wenyemisiba na matatizo mbali mbali ya kijamii.
Aidha Mhe. Othman amesema mbali na
hali hiyo, pia suala hilo linasaidia na linajenga matumaini ya kuwepo na
kuendeleza umoja na mshikamano miongoni mwa viongozi na wananchi sambamba na
kuwepo matumaini makubwa kwa wananchi kutoka kwa viongozi wao.
Amefahamisha kwamba umuhimu wa
ziara hizo pia ni viongozi kujifunza kwa uhalisia changamato za wananchi
walizonazo sambamba na kutafuta mbinu za pamoja katika kuzikabili na kuweza
kuzitatua changamoto hizo.
Hiyvyo Mhe. Othman amesema kwamba kufanya hivyo kwa viongozi ni kutekeleza
wajibu mkubwa walionao katika kuwafariji
na kuwapa matumini mema wananchi katika kuendeleza umoja miongioni mwa wananchi
na viongozi wao kwa ngazi mbali mbali.
Mhe. Othman amewataka wananchi na
viongozi kuendelea kuwa na umoja pamoja
subra kutokana na matatizo mbali mbali yanayowafika ikiwemo ugonjwa na misiba
na kumuomba mwenyezi mungu kuwarejeshea afya wale wote waliofikwa na mitihani ya
maradhi na kuendelea kuwaombea dua waliotangulia.
Amewataka viongozi kuendeleza mila hizo nzuri za kuwatembelea watu na
wagonjwa mbali mbali hasa katika kipindi
kama hiki cha mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani kwani ziara kama hizo ni alama
za kuwakumbusha katika wajibu wa kuwa pamoja wakati wa furaha na changamoto
mbali mbali .
Akizungunzia suala la nchi, Mhe.
Othman amesema kwamba viongozi wamekabidhiwa dhamana na wananchi na kwamba kwa
juhudi kubwa wamekua wakifanyakazi chini ya serikali ua
umoja wa kitaifa kwa kusimamia vyema na
kuwepo kwa matumaini ya kuondosha shida
mbali mbali za wananchi kupitia serikali hiyo ili na wengine watamani kuiga mfumo
wa serikali hiyo.
Mapema Mwenyekiti wa Chama hicho
mkoa wa Kaskazini A Kichama Mcha Rajab Haji, akitoa shukrani zake kwa Mhe.
Othman amesema kwamba viongozi na wananchi wamefarijika sana kwa kuwepo ziara
za namna hiyo kwa kuwa zinawaweka wananchi pamoja.
Naye Katibu wa Haki za Binaadamu na
Makundi Maalum wa Chama hicho Pavu Abdalla Juma, amesema kwamba ziara hizo
zinaleta faraja na matumaini kwa wananchi na kwamba viongozi wamekuwa wakifanya
kazi kubwa na kwamba ameweza kutembelea
zaidi nyumba 43 katika mkoa huo pekee.
Mhe. Othman tayari amefanya ziara
kama hizo katika Mkoa wa Kusini Unguja, Mjini Magharib na mikoa miwili ya Pemba
ambapo kesho anatarajiwa kukamilisha ziara yake hiyo katika wilaya ya Magharib
A na B.
Ziara hizo ni mwendelezo wa urithi
uliachwa na Mtangulizi wake Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad ambazo katika uhai wake alizifanya kila ifikapo
mwenzi mtukufu wa Ramadhani kuwatembelea wagonjwa, wenye misiba na shida
nyeingine mbali mbali katika visiwa vya Unguja na Pemba.
No comments:
Post a Comment