Habari za Punde

Serikali yageukia Viongozi wa Dini Mapambano dhidi ya Uhalifu

 

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Daniel Sillo akisalimiana na Mkuu wa Kanisa Kuu la Kiinjili na Kilutheri(KKKT),Askofu  Dkt.Alex Malasusa(kulia) wakati wa mazungumzo yaliyohusisha viongozi wa dini na serikali kuelekea katika mkakati wa kuunganisha nguvu ili kupambana na uhalifu,mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Gervais Nyaisonga (kulia) wakati wa mazungumzo yaliyohusisha viongozi wa dini na serikali kuelekea katika mkakati wa kuunganisha nguvu ili kupambana na uhalifu,mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa dini kutoka kulia ni Mchungaji Dkt.Barnabas Mtokambali, Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Gervais Nyaisonga na Mkuu wa Kanisa Kuu la Kiinjili na Kilutheri(KKKT),Askofu  Dkt.Alex Malasusa na kutoka kushoto ni Naibu Mufti wa Zanzibar,Mahmoud Mussa na Mufti Mkuu wa Tanzania,Sheikh Abubakar Zubeir wakati wa mazungumzo yaliyohusisha viongozi wa dini na serikali kuelekea katika mkakati wa kuunganisha nguvu ili kupambana na uhalifu,mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Na Mwandishi Wetu,Dodoma.                                                                                  

Katika kukabiliana na matukio ya uhalifu yanayotokea katika 

jamii tunayoishi Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani 

ya Nchi imefanya Kikao Maalumu na Viongozi wa Dini lengo 

ikiwa kuhusisha kundi hilo maalumu katika kudhibiti matukio 

ya uhalifu ikiwemo mauaji,mmomonyoko wa 

maadili,matumizi ya dawa za kulevya na matukio mengine 

yanayoweza kuvuruga amani ya nchi.


Akizungumza katika Kikao hicho kilichofanyika Makao 

Makuu ya wizara Mtumba jijini Dodoma,Waziri wa Mambo ya 

Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni amewaomba 

viongozi hao wa dini kuendelea kuisaidia serikali katika 

kudumisha amani na usalama,akiwaomba kutochoka kutoa 

ushauri kwa serikali katika kudhibiti matukio ya uhalifu 

yanayoweza kuvuruga amani ya nchi huku akikiri kuwepo kwa 

upungufu wa uhalifu nchini akiwaomba viongozi hao kuiunga 

mkono serikali katika adhma yake ya kumaliza kabisa uhalifu.


‘Wajibu wa Jeshi la Polisi ni kuhakikisha ulinzi wa raia na 

mali zao unaimarika na amani inatawala nchini ili kuwezesha 

wananchi kufanya kazi zao za kiuchumi na kijamii na katika 

kutekeleza wajibu huo Jeshi la Polisi ushirikiana na jamii na 

wadau wengine na katika kipindi cha Julai,2023 hadi 

April,2024 makosa makubwa ya jinai yaliyoripotiwa katika 

Vituo vya Polisi yamepungua kutoka 45,485 hadi 43,146 sawa 

na asilimia tano ikilinganishwa na kipindi kama hiki mwaka 

2022/2023,kwahiyo nawaomba viongozi wa dini mkaiunge 

serikali mkono katika sehemu zenu mnakotoka kukemea na 

kudhibiti uhalifu’ Alisema Waziri Masauni


Akizungumza wakati wa kikao hicho,Mufti Mkuu wa 

Tanzania,Sheikh Abubakari Zubeir aliipongeza  serikali kwa 

uamuzi wa kuhusisha viongozi wa dini katika mapambano 

dhidi ya uhalifu huku wakiitaka serikali kutochoka kuwaita 

yanapotokea matatizo mbalimbali ili kuendelea kuimarisha 

uhusiano huo.


‘Sina kumbukumbu kama tuliwahi kukaa hivi kujadili masuala 

ya uhalifu tangu wakati wa viongozi wetu wa zamani ila kwa 

hatua hii ya kuamua kutuita viongozi wa juu wa dini 

umefanya jambo la maana sana mheshimiwa Waziri na 

nikupongeze wewe na wenzako kwa wazo hili ambalo sasa 

linaenda kufungua milango ya mahusiano kati ya serikali na 

taasisi hizi za dini katika mapambano dhidi ya uhalifu.’ 

alisema Sheikh Zubeir


Akizungumzia usajili wa taasisi za kidini, Askofu wa Jimbo 

Kuu Katoliki Mbeya na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki 

Tanzania, Gervais Nyaisonga amesema serikali ipitie upya 

katiba za vikundi mbalimbali vya kidini kwani kupitia katiba 

zao ndio serikali itajua msingi wa shughuli za taasisi hizo za 

kidini ili kuepusha baadhi ya uhalifu ambao pia unatokea 

katika baadhi ya taasisi au vikundi vya kidini.


Naye Mkuu wa Kanisa Kuu la Kiinjili na 

Kilutheri(KKKT),Askofu Dkt. Alex Malasusa alisema 

wanaishukuru serikali kwani sasa wamepata mahali kama 

viongozi wa dini ambapo wanaweza kuzungumza na kuweka 

mikakati ya pamoja katika mapambano dhidi ya uhalifu na 

kukubaliana juu ya maazimio yaliyofikiwa ili kuona nchi 

inakua na amani na usalama.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.