Na Oscar Assenga, TANGA
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian leo ameungana na Waislamu mkoani Tanga kushiriki katika ibadaa ya Eid-alfitr iliyofanyika kwenye Msikiti wa Ijumaa Jijini Tanga huku akiwataka wakazi wa mkoa huo kuendelea kutenda matendo mema.
“Nimefikisha salamu za Rais Samia Suluhu ambaye anawatakia wote salamu za Eid Mbarak na anawaomba muendele kufurahia na kuendeleza matendo mema ambayo tuliyafanya kwenye mwezi wa ramadhani”Alisema
“ Jana Rais Dkt Samia Suluhu aliweza kutushika mkono wakuu wa mikoa wote na kutoa sadaka ya mbuzi kila kituo na kupelekea kwenye vituo vya watoto yatima ili watoto waliopo kwenye mazingira magumu wawaze kufurahia sikukuu hivyo tunaendelea kumuombea rais kilalaheri na mwenyezi mungu ampe umri na maisha marefu na Baraka tele”Alisema
No comments:
Post a Comment