Habari za Punde

(Z-NCDA) imeipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mkakati wake wa kupima afya kwa Jamii

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa  Muungano wa Jumuiya ya Maradhi Yasioambukiza Zanzibar  Dk Said Gharib Bilal akifungua Mkutano wa ushawishi na utetezi  na kubadilishana uzoefu huko Jumuiya hiyo Mpendae .
Baadhi ya washiriki wakimsikliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa  Muungano wa Jumuiya ya Maradhi Yasioambukiza Zanzibar  Dk Said Gharib huko katika  Jumuiya hiyo Mpendae .

Muungano wa Jumuiya ya maradhi yasioambukiza Zanzibar  (Z-NCDA)  imeipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mkakati wake wa kupima afya kwa Jamii  ili kupambana na maradhi yasioambukiza nchini.

Akitoa kauli hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Jumuiya hiyo, Dk Said Gharib Bilal katika Mkutano wa ushawishi na utetezi  na kubadilishana uzoefu juu ya kupambana na maradhi yasioambukiza katika Jumuiya ya Umoja wa watu wanaoishi na Maradhi yasioambukiza, Mpendae .

Amesema  mkakati huo ni hatua muhimu na ya kupongezwa, kwani utasaidia kugundua mapema magonjwa kama shinikizo la damu, kisukari, saratani na maradhi ya moyo ambayo yamekuwa yakiongezeka siku Hadi siku na kusababisha vifo.

Amesema juhudi za Serikali kupitia Wizara ya Afya, itasaidia wananchi kupatiwa tiba kwa haraka na kuokoa Maisha yao.

Aidha amesema kuwa  hatua hiyo ni muhimu katika kupambana na maradhi hayo jambo ambalo litasaidia  kupunguza ongezeko la maradhi  hayo.

Dkt Said ameahidi kuwa  Jumuiya hiyo itaendelea kushirikiana na  Wizara ya Afya ili  kuhakikisha watu Wanapatiwa elimu sahihi juu ya Maradhi hayo pamoja na njia ya kukabiliana nayo.

Nae Mwenyekiti  wa Jumuiya hiyo Louis H. Majaliwa alisema maradhi yasioambukiza yamekuwa kwa kasi hapa Zanzibar kutokana na wananchi kutokukubali kubadili mfumo wao wa maisha.

Hivyo aliitaka Jamii kujenga utamaduni wa kupima afya mara kwa mara ili  kugundulika tatizo  mapema na kupatiwa matibabu Kwa haraka .

Naye Meneja wa Jumuiya hiyo Haji  Khamis Fundi amesema kupitia mradi wa mkakati imeweza kuwapatia elimu ya maradhi yasioambukiza Wadau Mbali mbali Kwa lengo la kufikisha kwa Jamii wakiwemo Waandishi wa Habari wasanii watunga sera pamoja na watetezi dhidi ya maradhi ya kisukari.
 na maradhi yasioambukiza

Kwa Upande wa  watu wanaoishi na maradhi hayo ameishukuru Serikali Kwa kujenga vituo vya afya mbali mbali jambo ambalo limerahisishia  upatikanaji wa huduma za matibabu hayo .

Mkutano huo umehusisha  Wadau mbali mbali ikiwemo Madaktari , Waandishi wa Habari, watu wanaoishi na maradhi pamoja na Jumuiya wanachama.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.