Na Rajaba Mkasaba, Pemba
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa ufunguzi wa zahanati ya Kambi ya Ali Khamis iliyopo Pemba utasaidia kutekeleza lengo la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar la kuimarisha huduma ya afya nchini.
Hayo aliyasema wakati wa ufunguzi na makabidhiano ya zahanati ya Kambi ya Ali Khamis, iliyopo Mkoa wa Kusini Pemba ambayo imefanyiwa ukarabati mkubwa kwa msaada wa serikali ya Marekani.
Dk. Shein alisema kuwa kituo hicho ni kielelezo madhubuti cha mashirkiano kati ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Marekani, ambacho kitashiriki kikamilifu mikakati ya sekali ya kuinua huduma za afya hapa Zanzibar.
Alisema kuwa hatua hiyo inatokana na azma ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 ambayo pia, yalilenga kuwapatia wanyonge huduma ya afya ambayo kabla ya hpo walikuwa wahaipati.
Alieleza kuwa kabla ya hapo huduma za afya zilikuwa zikitolewa kwa ubaguzi mkubwa na kufanya wengi ya wananchi kukosa huduma hiyo ambapo baada ya Mapinduzi hal hiyo imegeuka na hivi sasa uduma hiyo inatolewa kwa wananchi wote bila ubaguzi.
Katika hotuba yake hiyo, Dk. Shein alisema kuwa huduma za afya kwa hapa Zanzibar zimeimarika kwa kiasi kikubwa ambapo kwa hivi sasa hakuna eneo ambalo linaweza kufikia kilomita tano bila ya kukuta kituo cha afya, Unguja na Pemba.
Alisema kuwa juhudi zinazochukuliwa hivi sasa na serikali ni kuhakikisha mkazo mkubwa unawekwa katika kuinua sekta hiyo ya afya kwa lengo la kuwapa wananchi huduma iliyo bora zaidi na kusisitiza kuwa kituo hicho pia, kitahudumia wananchi.
Akieleza miongoni mwa mikakati iliyowekwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Shein alisema ni pamoja na kuanzisha huduma za upasuaji wa moyo, huduma za figo na maradhi ya saratani hapa hapa Zanzibar badala ya huduma hizo kufuatwa nje ya nchi
Aidha, Dk. Shein alisema kuwa n azma ya serikali kuziongezea nguvu ikiwa ni pamoja na kuongezea wafanyakazi, vifaa na utaalamu wa kisasa hospitali za Wete na Mkoani ili ziwe hospitali za Mkoa
Pia, alisema vituo viwili vya afya ambavyo ni Vitongoji na Micheweni vitapandishwa daraja ili viwe hospitali za Wilaya kwa lengo la kuimarisha huduma hiyo ya afya na kueleza kuwa hatua za serikali kuunga mkono uimarishaji wa huduma za afya Zanzibar n mnasaba wa kufikia lengo hilo.
Pamoja na hayo, Dk. Shein alitoa wito kwa wananchi kutumia fursa ya kuwepo kwa kituo hicho kwa kwenda kuangalia afya zao katika kituo hiho ikiwa ni pamoja na kupima virusi vya ukimwi.
Nae Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Uchum Tanzania, Mhe.Dk. Hussen Mwinyi alisema kuwa kabla ya ukarabati kituo kilikuwa na uwezo wa kutibu wagonjwa takriban 200 kwa mwezi na baada ya ukarabati kituo kina uwezo wa kutibu wagonjwa 600 kwa mwezi.
Pamoja na kutoa matibabu ya magonjwa ya ujumla kituo pia, kinahudumia wagonjwa waloathirika na VVU/UKIMWI.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Alfonso Lenhardt naye alieleza lengo la serikali yake la kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika sekta za maendeleo.
Balozi huyo alisema kuwa hospitali hiyo pia,i tatoa huduma kwa akina mama na watoto na kusisitiza kuwa mahusiano mazuri yaliopo kati ya Zanzibar na Marekani yataimarisha zaidi uendelezaji wa miradi ya maendeleo.
Zaidi ya shilingi milioni 200 zimetumika katika ukarabati wa kituo hicho cha afya.
Labels
- .
- `
- 8
- AFYA
- AFYA.
- AJALI
- BIASHARA
- BURUDANI
- DINI
- ELIMU
- FILAMU
- HABARI
- HARUSI
- HOSPITALI
- I
- JAMII
- KATUNI
- Kii
- KILIMO
- KIMATAIFA
- KITAIFA
- Ku
- MAGAZETI
- Mahkamani
- MAISHA
- MAKALA
- MAKALA AFYA.
- MAKALA.
- MATUKIO
- MATUKIO.
- MICHEZO
- MITAANI
- MIUNDOMBINU
- MSAADA
- Ok
- SIASA
- TANGAZO
- TAWA YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI
- TEKNOLOJIA
- UCHUMI
- UTAFITI
- UTALII
- VIDEO
- VIJANA
- VISA INTERNATIONAL YAZINDUA TAWI TANZANIANa Mwandishi wetu 16.07.2025DAR ES SALAAM
- WEZI
Tafsiri ya Lugha
Popular Posts
-
Mtaalamu wa lugha ya Alama Masika Khamis Ali akitoma maelezo kwa Wananchi wa makundi maalumu wakati wa ufungaji wa Mkutano wa Kampeni wa Cha...
-
Wajasiriamali mbalimbali kisiwani pemba wakipata mafunzo ya usindikaji wa matunda kutoka kwa Mtaalam akitowa mafunzo hayo kwa wajasiria...
-
Jeshi la Polisi limewataka wananchi kutokuwa na hofu ya ulinzi na usalama wao siku ya uchaguzi Oktoba 29, 2025 na limewasihi wakapige kura n...
-
Shamra shamra wakati akiwasili Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Ujumbe wa Misheni ya Uangalizi wa Uch...
-
Wachezaji wa Timu ya Chipukizi wakishangilia bao lao ya kusawazisha katika mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar PBZ dhidi ya Timu ya Uhamiaji ...
-
Na Mwandishi Wetu WMJJWM- Njombe Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Mkaundi Maaalum Dkt. John Jingu, amewataka...
-
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Taifa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete a ki zuru kaburi l a Marehemu Mohamed Seif Khatib, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa...
-
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Nishati, Bi. Ziana Mlawa (Wa tatu kutoka kulia mstari wa nyuma) akiwa Katika pich...
-
Dar es Salaam. 28-10-2025 Tanzania Bloggers Network (TBN) inatoa pongezi za dhati kwa Watanzania wote, wagombea, vyama vya siasa, Tume Huru ...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
BLOGU RAFIKI
-
-
Rais na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan apiga Kura katika Kituo cha Ofisi ya Kijiji Chamwino mkoani Dodoma - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) M...1 day ago
-
Elimu : Bajeti za Elimu Zisipuuzwe wakati wa misukosuko ya Kiuchumi na Kisiasa Duniani - Kikwete na Malala Waonya. - Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai, wameonya juu ya mwenendo hatarishi duniani wa kupunguza au ku...1 week ago
-
MAHOJIANO YA TAUSI SUEDI NA AMRI NGOYE KUHUSU CSI KUPITIA KWANZA PRODUCTION NCHINI MAREKANI - Pata habari motomoto kupitia facebook kwa kulike huu ukurasa wetu https://www.facebook.com/pages/Pamojapureblogspotcom/312633955485619?ref=hl7 years ago
Marafiki Duniani
Popular Posts
-
Mwili wa Marehemu unatarajiwa kuwasili Zanzibar majira ya mchana kwa Ndege na kuendelea na taratibu za Maziko yatafanyika katika Mtaa wa...
-
The United Republic Of Tanzania National Examination Council of Tanzania Form Four Examination Results 2017/2018 The National E...
-
Makamanda wa JWTZ wakiwa wamebeba mwili wa Marehemu Waziri Kiongozi wa Kwanza wa Zanzibar na Brigedia Jenerali Mstaaf Ramadhani Haji Faki...
-
Na Miza Kona/Rahma Khamis Maelezo-Zanzibar Jumla ya wanafunzi 16,744 wamechaguliwa kuendelea masomo ya kidatu cha tatu kati ya wanafun...
-
Bwana Harusi Lusajo Sajent Mwangambaku (kushoto), akiwa katika pozi na mke wake Neema Stanley Matowe katika hafla yake ya ndoa iliyofa...
-
Mama mjazito akihangaika na hatimaye kupoteza maisha kutokana na mimba za utotoni..Video ipo hapo chini baada ya maelezo mafupi
-
Hutuba ya Mhe Waziri wa Afya Nd. Mahmoud Thabit Kombo kwa Waandishi wa Habari Katika Maadhimisho ya Siku ya Malaria Dunia Zanzibar, 22...
-
Madawa na Maji vilivyokabidhiwa na Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, kwa Wizara ya Afya kwa ajili ya Kambi za K...

No comments:
Post a Comment