Habari za Punde

Balozi Seif Ali Iddi, Akibidhi Vikundi vya Wanawake Nyenzo za kazi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akitowa nasaha zake kwa Wanawake  Wanavikundi wa Jimbo la Malindi wakati walipofika kutowa vifaa vya kujiendeleza vilivyotolewa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shein na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais Mama Asha Balozi Seif, makabidhiano hayo yamefanyika katika Tawi la CCM Malindi.  


Khadija Seif akisoma risala kwa niaba ya Wanawake wa Jimbo la Malindi wakati wa hafla ya kukabidhiwa vitendea kazi kwa vikundi vya Wanawake wa Jimbo hilo zilizofanyika katika tawi la CCM Malindi.  
Katibu wa Wake wa Wawakilishi na Wabunge Zufura Mgeni Mwalim akisoma majina ya Wanavikundi ili kukabidhiwa vifaa vyao kwa ajili ya kuzalisha mali katika vikundi hivyo ili kujiegezea kipato katika kazi za amali.
Msoma Utenzi Farida Rajab akisoma moja ya utenzi katika hafla ya kutowa  vifaa vya Wanavikundi wa jimbo la Malindi iliofanyika katika ukumbi wa tawi la CCM Malindi Zanzibar.  
Wanawake wa Viongozi wakisikiliza Makamu wa Pili wa Rais akitowa nasaha zake kwa Wanavikundi wa Mji mkongwe baada ya kukabidhi vitendea kazi vya vikundi hivyo, vilivyotolewa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Shein na Mke wa Makamu wa Pili Mama Asha Balozi Seif kwa vikundi hivyo kujiendeleza kiuchumi na kujiogezea kipato chao.  
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimkabidhi nyezo Katibu wa Kikundi cha Mwanzo Mgumu cha Wadi ya Mchangani Bishara Hamad.
Mwenyekiti wa UWT Jimbo la Mji Mkongwe Fatma Hamza akitowa neno la shukrani kwa msaada waliopata kwa vikundi vya jimbo lao baada ya makabidhiano hayo yaliofanyika tawi la CCM Malindi.
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif Iddi, akitowa nasaha zake kwa Wanawake wa Vikundi vya jimbo la Mtoni katika tawi la CCM Mtoni, na kuwataka wasiwe wakiwa kwa kutokuwa na mbunge na mwakilishi wa CCM katika jimbo hilo kwani wao ndio walezi wao mna wako tayari kutowa msaada wakati wowote wakiwa na shinda katika vikundi vyao.    

Makamu wa Pli wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimkabidhi fedha tasilim na vifaa vya kufugia kuku Katibu wa Kikundi cha Mshikamano Daima -Mtopepo Neema Ali, makabidhiano hayo yamefanyika katika tawi la CCM Mtoni.
Makamu wa Pli wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimkabidhi fedha tasilim na vifaa vya kufugia kuku Katibu wa Kikundi cha Imania Corparative -Welezo Asha Mohammed, makabidhiano hayo yamefanyika katika tawi la CCM Mtoni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.