Habari za Punde

Dk Shein afanya uteuzi, amteua mwenyekiti wa bodi ya uhaulishaji Ardhi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemteuwa Juma Khamis Juma kuwa Mwenyeikiti wa Bodi ya Uhaulishaji Ardhi,Zanzibar.

Kwa mujibu wa Taarifa iliotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Dkt Abdulhamid Yahya Mzee ameeleza kuwa uteuzi huo ni kwa mujibu wa uwezo aliopewa Rais chini ya Sheria Namba 8 ya mwaka 1994 kama ilivyorekebishwa Sheria namba 10 ya mwaka 2007 ya uhaulishaji wa Ardhi-Zanzibar.

Uteuzi huo unaanza leo tarehe 30Julai, 2012

2 comments:

  1. Baada ya juhudi kubwa za wawakilishi hatimae Mwenyekiti wa bodi ya uhaulishaji ndio ameteuliwa.

    Kwa kipindi cha takriban miezi sita, Z'bar imekaa bila ya chombo halali cha kusimamia'transfer of properties' halafu eti watu wanadai kua matatizo yetu yanatokana na muungano.

    ReplyDelete
  2. Right, first we have to deal with our own issues and then to look ahead

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.