UONGOZI wa Jimbo la Kitope, unakusudia kuimarisha sekta ya michezo kwa lengo la kuwawezesha vijana wa jimbo
Mbunge wa Jimbo
Balozi Seif aliwaeleza wawakilishi wa timu hizo ambazo ni Kitope United, African Boys, Home Boys na Kombora, kuwa uamuzi wao wa kufikiria kuanzisha timu moja imara ya jimbo ni faraja kwa viongozi, na kwamba utarahisisha upatikanaji wa vifaa na misaada kwa wepesi zaidi.
Aliahidi, kwa kuwa yeye ni kiongozi wao wa jimbo, atahakikisha sekta ya michezo
inapata nguvu zaidi kutokana na umuhimu wake uliojichomoza hivi karibuni
wa kutoa ajira endapo vijana hao watajituma vilivyo.
Aidha aliahidi kuzungumza na wafadhili mbalimbali wa michezo, ili
kuona namna gani wanaweza kusaidia uimarishaji wa uwanja wa uhakika na wa
kisasa ndani ya jimbo hilo.
Alisema suala hilo litakwenda sambamba
na upatikanaji wa vifaa vya michezo ikiwemo mipira, nyavu, magoli na jezi
ambazo alisema zimo ndani ya uwezo wake kulingana na utaratibu
aliokwishauanzisha tokea alipoanza kuliongoza jimbo hilo .
Aliwataka kuanza maandalizi ya msingi kwa ajili ya ujenzi wa jingo la
klabu, na kusema atahakikisha anasaidia
nguvu za unyanyuaji jengo kwa hatua ya matofali na kuangalia mbinu za
kuendeleza ujenzi huo.
Mapema wanamichezo hao walimueleza Balozi Seif matatizo
yanayowakabili katika katika harakati zao za kuendeleza michezo ambayo yamekuwa
yakipunguza kasi yao
ya ufanisi, ikiwa ni pamoja na uhaba wa vifaa vya michezo, ujenzi wa jengo la klabu
pamoja na uanzishwaji wa mashindano ya Kombe la Mbunge.
Katika kikao hicho, Balozi Seif Ali Iddi alikabidhi seti ya jezi na fedha
taslimu kwa timu ya soka ya Kitope United inayojiandaa na usajili kwa ajili
ya mashindano yajayo.
No comments:
Post a Comment