Joseph Ngilisho,Arusha
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la
Anglikana nchini,Dk. Valentino Mokiwa amelitaka kanisa hilo kukataa
fedha chafu zinazotolewa kama sadaka na mafisadi wanaotumia mgongo wa makanisa
kujisafisha.
Askofu Mokiwa aliyasema hayo katika ibada maalumu ya shukrani iliyofanyika kanisa la Anglican dayosisi ya Mount Kilimanjaro.
Ibada hiyo imefanyika baada ya
kumalizika mgogoro wa muda mrefu uliolikumba kanisa hilo na kusababisha Askofu
wa kanisa hilo mkoa wa Arusha,Stanley Hotay kupingwa mahakamani.
Dk.Mokiwa alisema kumeibuka
tabia zisizofaa kwa baadhi ya viongozi wa dini kuogopa kuwakemea mafisadi wa
makanisa baada ya kukubali kupokea fedha zao huku wakijua kabisa wanakiuka
sheria za kanisa.
Alisema iwapo mafisadi hao wataachwa
watambe makanisani ni wazi kanisa litagawanyika kutokana na wao kutaka
kuliendesha watakavyo.
Alilitaka kanisa hilo kuacha
tabia ya kuwa omba omba badala yake lijijengee uwezo wa kujitegemea kwa kubuni
miradi mbalimbali ikiwemo kuanzisha shule na hospitali hatua ambayo itasaidai
kuondoa fedha chafu zinazopenyezwa na mafisadi kanisani.
Katika hatua nyingine askofu
Mokiwa aliwataka waumini wa dini hiyo kuacha kuyashabikia baadhi ya magazeti
ambayo yanaandika vibaya habari zake.
Naye askofu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Mount Kilimanjaro,Stanley Hotay aliliomba kanisa hilo kuendelea kudumisha amani na kushirikiana kwa pamoja na kusahau yote yaliyopita.
No comments:
Post a Comment