Na
Hafsa Golo
SERIKALI
ya Mapinduzi Zanzibar imepiga hatua katika kutanua sekta ya elimu mjini na vijijini ambapo jumla
ya wanafunzi 361,610 wanapatiwa elimu katika taasisi mbali mbali ili taifa
liweze kuwa kuzlisha wataalamu wake katika
fani mbali mbali.
Akizungumza
juu ya maendeleo hayo,Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamuhuna
alisema jukumu hilo
limeanza kuonesha dalili ya kufikiwakidogo kidogo kulingana na maendeleo ambayo
sekta ya elimu imetapata katika miaka 48 ya elimu bila malipo.
Alisema taasisi matumaini hayo yamekusanya nyanja
nyingi na inaonekana dhahiri kwamba taasisi zinazotoa elimu kwa wanafunzi hao zimefikia 713, zikiwemo Skuli
za Maandalizi 253, skuli za Msingi kamili 194, Skuli za Sekondari kamili 107,
Skuli za mchanganyiko, Msingi na sekondari pamoja 149, Vyuo vikuu vitatu.
Alifahamisha
kuwa uandikishaji wa wanafunzi katika ngazi ya elimu ya maandalizi imefikia
asilimia 34.4, na ngazi ya msingi asilimia 121.5,ngazi ya sekondari asilimia 67
sambamba na uwiyano kati ya wanafunzi wa kiume na wanafunzi wa kike wamekuwa
wakilingana katika ngazi za msingi na sekondari.
Alisema
hatua hiyo ya maendeleo imefikiwa kutokana na ushirikiano makubwa yaliopo kati
ya wananchi na serikali kwani wananchi wamekuwa wakitoa michango katika maeneo mbali mbali hasa kwa ujenzi wa madarasa.
"Pia
ninawapongeza kwa juhudi kubwa kuhakikisha watoto wenu wanaandikishwa na
wanahudhuria masomo katika skuli zilizokaribu na maeneo munayoishi,ninawaomba
tuendelee kushirikiana ili sekta yetu ya elimu iweze kupata maendeleo
zaidi."alisema
Akizungumzia upande wa elimu ya juu, alisema
kuwa hatua ya maendeleo imefikiwa kwani hivi sasa zipo taasisi nne zinazotoa
elimu ya Chuo kikuu,akizitaja taasisi hizo alisema Chuo kikuu cha Taifa cha
Zanzibar,Chuo Kikuu cha Zanzibar, Chuo Kishirikishi cha Elimu Chukwani na
Taasisi ya Fedha iliyopo Chwaka.
Aidha, alisema pamoja na mafanikio makubwa
yaliofikiwa katika sekta ya elimu, bado yapo matatizo mbali mbali yanayoikumba
sekta ya elimu yakiwemo uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi, uhaba wa vikalio
na vifaa vya maabara.
Shamuhuna
alisema azma ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutatua matatizo hayo hatua
kwa hatua, ikiwa moja wapo ni kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Marekani
(USAID) ambapo imeanza kutekeleza mradi wa TZ21 wa kupatiwa kompyuta kwa
kuhifadhia kumbukumbu na kutumiwa kwa kufundishia na kujifunzia.
Kutokana
na kiwango hicho cha wanafunzi ambao wamekuwa wakipata huduma muhimu ya elimu
katika taasisi mbali mbali alisema ni jambo muhimu kwa taifa
na yataweza kufikiwa malengo
yaliokusudiwa.
No comments:
Post a Comment