Habari za Punde

Serikali yatoa mkono wa pole kwa waathirika wa maafa ya kuunguliwa kwa moto , Tumbe

 
WAZIRI wa Nchi Afisi ya Makamu wa pili wa Rais, Zanzibar Mohamed Aboud Mohamed akizungumza na wananchi wa Tumbe Wilaya ya Micheweni, ambao walikumbwa na maafa ya kuunguliwa nyumba zao moto hivi karibuni, ambapo Waziri Aboud alikabidhi ubani wa shilingi milion tano na laki moja kutoka kwa Rais wa Zanzibar dk Ali Mohamed Shein , kulia na mwakalishi wa nafasi za wanawake Asha Bakar Makame (picha na Haji Nassor, Pemba)

 
Nyumba zilizoungua moto hivi karibuni, huko shehia ya Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, ambapo nyengine zilibakia kuta na nyengine kusambaratika kabisa, (picha na Haji Nassor, Pemba)


WAZIRI wa Nchi Afisi ya Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Mohamed Aboud Mohamed, akimkabidhi Riziki Hamad Ali wa shehia ya Madungu shilingi laki tano na nusu, za mkono wa pole kutoka kwa rais wa Zanzibar dk Ali Mohamed Shein, ambapo Riziki ni mmoja tu kati ya wananchi kadhaa Kisiwani Pemba, hivi karibuni waliokumbwa na maafa ya kuunguliwa nyumba zao na moto uliodaiwa kuwa wa maajabu (picha na Haji Nassor, Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.