Habari za Punde

Shamuhuna apokea msaada wa madeski

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna (wamwanzo kulia)akitoa hotuba katika sherehe za kukabidhiwa Madarasa 17yaliofanyiwa Ukarabati pamoja na Madawati180 yaliotengenezwa ikiwa ni msaada kutoka Shirika la Maendeleo la KOICA kutoka Korea,kwa ajili ya Skuli ya kukabidhiwa Madarasa 17yaliofanyiwa Ukarabati pamoja na Madawati180yaliotengenezwa Chuini ilio kaskazini Unguja kushoto yake ni Meneja wa Shirika la KOICA Seung Beom Kim.
 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna akimkabidhi Cheti cha Shukurani na Ushirikiano Meneja wa Shirika la KOICA kutoka Korea Seung Beom Kim.katika Hafla ya Sherehe za kukabidhiwa Madarasa 17yaliofanyiwa Ukarabati pamoja na Madawati180yaliotengenezwa na Shirika hilo kwa ajili ya Skuli ya Chuini ilio kaskazini Unguja
 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna (Kushoto)akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Abdalla Mzee Abdalla katika Sherehe za kuwatunuku vyeti Walimu wanaofundisha Somo la Kingereza waliomaliza Mafunzo yao ya kuwajengea Uwezo wa kutumia Lugha hio katika Ufundishaji hapo Kituo cha Walimu cha Taifa Nkruma

 Mwalimu Salum Omar kutoka Skuli ya Machui Zanzibar akionyesha namna ya kuwafundisha Watoto Somo la Kingereza kwa Kutumia Kingereza na mbinu mbalimbali za Usomeshaji walizojifunza katika mafunzo yao yaliochukua muda wa siku 20 hapo Kituo cha Walimu cha Taifa Nkruma.
 Mwalimu Teresia Husein kutoka Skuli ya Kibele Zanzibar akionyesha namna ya kuwafundisha Watoto Somo la Kingereza kwa Kutumia Kingereza na mbinu mbalimbali za Usomeshaji walizojifunza katika mafunzo yao yaliochukua muda wa siku 20 hapo Kituo cha Walimu cha Taifa Nkruma.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna (Kushoto)akikabidhiwa Madawati 180 na Meneja wa Shirika la KOICA kutoka Korea Seung Beom Kim kwa ajili ya Skuli ya Chuini ilio Kaskazini Unguja.

Picha zote na Yussuf Simai, Maelezo

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.