KUSIMAMIWA
ipasavyo kwa majukumu ndani ya sekta ya
habari kwa kiasi kikubwa kutaweza kusaidia vyombo vya habari kutekeleza dhamana
zake pamoja na kujua wajibu wake ili kuleta maendeleo katika sekta hiyo.
Akizungumza
katika mkutano uliojumuisha wamiliki mbali mbali wa vyombo vya habari, Waziri wa Habari Utamaduni, Utalii
na Michezo Zanzibar, Said Ali Mbarouk alisema
wizara yake ina jukumu kubwa la kusimamia sekta ya habari ili kuhakikisha lengo
linafikiwa.
Alisema
wizara ina kazi kubwa ya kusimamia sera ya habari na utangazaji kwa kuitekeleza pale ambapo wakiona ina upungufu
kwa lengo la kufanya tathmini ili kuirekebisha kwa pamoja.
Waziri
huyo alisema ni wakati sasa kwa sekta ya habari kupiga hatua kubwa katika
ukanda wa Afrika Mashariki kutokana na kwamba Zanzibar ina historia pana katika sekta hiyo
hali ambayo itasaidia pia kurejesha heshima ya vyombo vya habari.
Alisema
nchi inapokosa uhuru wa habari huwa hakuna maendeleo hivyo ni vyema kukabiliana
na changamoto zilizopo ili kulinda hadhi
ya habari na upatikanaji wa habari hizo.
Sambamba
na hayo ameviomba vyombo vya habari kupanga mikakati ambayo itaratibiwa kati
yao na Wizara kwa lengo la kuendeleza sekta hiyo kielimu, kifikra na iweze
kutumika katika kuleta mageuzi ya ulimwengu.
Akichangia mada mmoja wa washiriki wa kikao hicho Kaimu Mkuu wa
Chuo cha habari Zanzibar, Rashid Omar alisema ni jambo la msingi kufanyiwa mapitio
sera na sheria ya utangazaji kutokana na kutumia vibaya lugha ya kiswahili
wakati wa uwasilishaji wa kazi zao.
Amevitaka
vyombo vya habari vya binafsi na serikali
kufanya utafiti wa kina wakati wa kukidhi mahitaji ya wafanyakazi kwa
kuzingatia mazingira na taaluma waliyonayo.
Nae
Hafidh Kassim alisema serikali inavipa mzigo mkubwa sana vyombo vya binafsi katika suala la
kuajiri pamoja na kutozwa kodi kubwa jambo ambalo linapelekea kuzorotesha
mwenendo mzima wa kubadilisha mitambo yake kutoka katika mfumo wa analogia na kwenda digitali.
No comments:
Post a Comment