Joseph
Ngilisho, Arusha
ZANZIBAR
zimewakaribisha wahisani katika sekta ya
kilimo, kusaidia wakulima wadogo kuboresha kilimo chao ili taifa liweze kuwa na uhakika wa chakula na kukabiliana na
umasikini.
Akizungumza
katika mkutano wa mapinduzi ya kilimo mjini Arusha, Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi alisema wakulima wa Zanzibar kama walivyo wakulima
wengine wadogo wanakabiliwa na tatizo la matumizi ya zana duni za kilimo, na
ukosefu wa mbegu za kisasa.
Alisema
ingawa serikali ya Zanzibar
imekuwa na programu mbali mbali za kusaidia sekta ya kilimo lakini inakabiliwa
pia na tatizo la ardhi hasa kutokana na ongezeko la watu.
Hata
hivyo, alisema licha ya uchache wa ardhi lakini hiyo iliyopo kama itatumiwa
vizuri hasa kwa zao za karafuu, Zanzibar
itakuwa na mafanikio makubwa.
Hivyo, alisema Zanzibar
inafungua milango kwa wawekezaji wa ndani na wa kigeni kuwekeza katika sekta ya
kilimo.
Balozi
Seif alisema wakuliwa wadogo wakiwezeshwa wanaweza kuzalisha kwa kiwango
kikubwa na kuipunguzia serikali kuagiza chakula kutoka nje.
Kwa
upande wake Makamu wa Pili wa Rais wa
Burundi, Gabriel Ntisezerana, alisema
Burundi imefanikiwa kuwa na ardhi bora
yenye rutuba lakini bado haijatumika ipasavyo katika kusaidia sekta ya kilimo.
“Bado
wakulima wetu wadogo wanakabiliwa na matatizo ya kutokuwa na zana bora za
kilimo na matumizi mazuri ya pembejeo,"alisema Ntisezerana.
Mkutano
huo, ulioandaliwa na taasisi ya mapinduzi ya kijani(AGRA) unaendelea katika hoteli ya Ngurdoto
mjini Arusha na unashirikisha wataalam wa sekta ya kilimo na wadau wengine
zaidi ya 1200 toka bara la Afrika na nje ya Afrika.
Wakati
huo huo Mwanzilishi wa Taasisi ya Mapinduzi ya Kijani barani
Afrika(AGRA),ambaye pia ni mke wa tajiri mkubwa duniani, Bill Gates, Melinda
Gates, ameimwagia sifa Tanzania,kutokana
na kuwa na mikakati madhubuti ya kuimarisha
sekta ya kilimo.
Akizungumza
katika mkutano wa pili wa mapinduzi ya kijani barani Afrika,katika hoteli ya
Ngurdoto Melinda Gates alisema,Tanzania ni
moja ya mataifa ambayo yanatarajiwa kuwa na maendeleo makubwa katika sekta ya
kilimo.
Alisema
alitembelea bara la Afrika kwa mara ya kwanza miaka 19 iliyopita na alifika
Tanzania na tangu wakati huo, kilio kikubwa cha wananchi hasa akina mama ni
umasikini ambao unachangiwa na kilimo duni.
Alisema
taasisi yake, imekuwa ikisaidia katika kilimo na sekta ya afya kwa kutambua
umuhimu wa sekta hizo katika kusaidia vita dhidi ya umasikini barani Afrika.
Melinda
alisema ni wajibu wa serikali za Afrika kuwasaidia wakulima, kulima mazao
ambayo yahawezi kuathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi na hilo
litawezekana kama kukifanyika tafiti za
kutosha katika sekta ya kilimo.
Hata
hivyo, alisema ni vyema wakulima wadogo wapewe uhuru wa kuchagua kulima mazao
ambayo wao wanayamudu na rahisi kwao kama
kilimo cha mihogo.
Alisema
msaada ni muhimu kwa wakulima wadogo, kwani wengi ambao wanajihusisha na kilimo
vijijini ni akina mama, ambao malengo yao
makubwa yamekuwa ni kupata fedha za kusomesha watoto wao na pia kuwahudumia
kiafya.
Hata
hivyo, alieleza kuridhishwa na watendaji wa AGRA kutokana na kuwa na program mbali mbali
za kusaidia sekta ya kilimo barani Afrika na sasa wamefikiwa zaidi ya wakulima
wadogo milioni moja.
Awali
Rais wa AGRA, Jane Karuku akizungumza katika mkutano huo,alisema taasisi hiyo
kwa kushirikiana na serikali kadhaa barani Afrika na taasisi binafsi imeweza
kusaidia sekta ya kilimo, hasa katika upatikanaji mbegu bora na masoko.
Alisema
bara la Afrika bado linahitaji uwekezaji mkubwa katika sekta ya kilimo, ili
kuwa na uhakika wa chakula la lishe na hilo litawezekana kama wakulima wadogo
hasa wa vijijini wakisaidiwa katika kupata pembejeo,miundombinu bora ya
kuwafikia na masoko.
Rais
huyo, alisema taasisi hiyo, itaendelea kusaidia miradi kadhaa ya kilimo nchini
Tanzania na maeneo mengine, ikiwepo pia kusaidia taasisi za utafiti na mbegu
ili kuweza kuwasaidia wakulima hasa wa vijijini.
No comments:
Post a Comment