Habari za Punde

Viongozi wa Uamsho wakataliwa dhamana tena


Kesi ya inayowakabili viongozi wakuu wa Jumuiya ya Uamsho iliyoendeshwa leo katika Mahakama kuu ya Vuga mjini Zanzibar imebainisha kulikataa ombi la dhamana na kupelekea Viongozi hao kurudi tena rumande.

Washtakiwa hao walifikishwa Mahkamani hapo mnamo majira saa mbili na nusu asubuhi huku wakiwa chini ya ulinzi mkali uliokuwa ukiongozwa na gari tatu za FFU pamoja na baadhi ya askari wa vikosi vya KMKM.
Katika kesi hiyo, Jaji Mkusa Sepetu amelazimika kulikataa ombi la dhamana kwa kudaiwa ya kwamba halikufuata taratibu sahihi za kisheria, hivyo Mahakama imewataka Mawakili wa wateja hao kufuata taratibu zilizo sahihi juu ya ombi lao la kupatiwa dhamana viongozi hao.

Kwa upande wa utetezi wa washtakiwa hao kimsingi hawakufurahishwa na maamuzi yaliyoamuliwa na Mahakama hiyo ya kulitupilia mbali ombi hilo la dhamana kwani wamesema hoja iliyotolewa uamuzi si miongoni mwa hoja iliowasilishwa kwa DPP
 
Kimsingi wamesema ni hoja iliyoibuliwa na Mahakama wenyewe jambo ambalo linawapa mashaka mawakili hao.
Aidha wamesema kuwa wallipanga kuwasilisha ombi jipya leo hii la kudai dhamana kwa wateja wao lakini kutokana na muda kutokuruhusu kwa siku ya leo wameamuwa kujipanga upya zaidi na kuwasilisha maombi hayo hapo kesho.
Kesi hio itasikilizwa tena mnamo tarehe 3/1/2013

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.