Na Kauthar Abdalla
MWENYEKITI wa Baraza la Biashara Zanzibar, Dk. Ali Mohamed
Shein ataongoza mkutano wa baraza hilo
utakaojadili suala la ubia na uwekezaji katika sekta ya viwanda nchini.
Mkutano huo ambao utawakutanisha wataalamu wa masuala ya
viwanda nchini na nje ya nchi utafanyika katika ukumbi wa salama hoteli ya
Bwawani kesho.
Katibu Mtendaji Baraza hilo, Ali Vuai aliyasema hayo
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za baraza hilo Kinazini mjini Zanzibar.
Alisema mkutano huo utawakutanisha pamoja wadau kutoka sekta
za umma na binafsi kwa lengo la kujadili
mambo muhimu ya maendeleo ya biashara kwa manufaa ya serikali na wajasiriamali.
Alisema suala la ubia na uwekezaji katika viwanda linaweza
kuleta maendeleo makubwa kwa Zanzibar.
Aidha alisema sekta ya viwanda iko nyuma sana hivyo mkutano huo utakuwa fursa muhimu
wa kuandaa mikakati ya kuhakikisha viwanda vinafufuliwa na vyengine vipya
vinaanzishwa.
Katibu huyo alisema nchi haiwezi kuwa
na uchumi imara bila ya kuwa na viwanda bora ambavyo pia vitatengeneza
fursa mpya za ajira nchini.
Alifahamisha kuwa
Baraza pia litatoa fursa kwa sekta binafsi kutoa kero zao ili Serikali
ijue majukumu katika utendaji wa sekta hiyo pamoja na kutoa fursa kwa wajasiria
mali
kutangaza na kuuza bidhaa zao.
Hata hivyo alielezea kuwa wana lengo la kuangalia mwenendo
mzima wa viwanda ili kujua Zanzibar
ina mwelekeo gani wa kimaendeleo.
No comments:
Post a Comment