Na
Mwantanga Ame
SERIKALI imetakiwa kuacha kitumia wakaguzi
binafsi katika kufanya ukaguzi wa mahesabu katika mashirika yake na badala yake
watumie wakaguzi wa serikali walio chini ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
Mwakilishi
wa Amani, Fatma Mbarouk aliyasema hayo wakati akichangia mswada wa sheria wa kuanzisha shirika
la meli Zanzibar, katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea mjini Zanzibar.
Mwakilishi
huyo alisema serikali inapaswa kuliangalia suala hilo kutokana na kuzoeleka kwa mashirika mengi yaliopo kuamua
kufanya ukaguzi kwa kuyatumia makampuni binafsi jambo ambalo limekuwa
likichangia uchelewaji wa kueleweka mahesabu ya serikali.
Alisema
mashirika mengi yamekuwa yakifanya ukaguzi wake kuanzia Januari hadi Disemba lakini serikali imekuwa
ikifanya hivyo kati ya mwezi Julai jambo ambalo linaweza kuleta migongano ya
kiutendaji.
Alisema
kwa vile Mkaguzi wa serikali ametajwa ndani ya katiba ya Zanzibar , ni vyema
akapewa hadhi ya kuyakagua mashirika badala ya kuendelea kutumia wakaguzi
binafsi wakati serikali imekuwa ikiajiri na kuwasomesha wataalamu wa fani hiyo.
Alisema
kuyatumia makampuni binafsi katika kufanya ukaguzi wa serikali kunaweza
kukasababisha usumbufu kwa kamati za baraza la Wawakilishi.
Alisema
kuja kwa mswada huo utawezesha kulifanya shirika la meli, kuwa mfano bora
katika uendeshaji kwa kujipangia shughuli zake na kuachwa lijiendeshe wenyewe
kwani mfumo wa sasa hauwezi kulifanya kuwa bora kutokana na kutegemea mkono wa
serikali kujiendesha.
Aliseaama
kazi kubwa inayotakiwa kufanywa ni viongozi wa wizara kutoa mamlaka kamili kwa
shirika hilo.
Nae
Mwakilishi wa Kiwani, Hijja Hassan Hijja akitoa maoni yake alisema ni lazima
mashirika ya umma yawe na Idara za ukaguzi kwani baadhi ya mashirika yanakwepa hilo ili kuweza kufuja mali za serikali.
Aidha,
Mwakilishi huyo aliiomba wizara husika kuona uteuzi wa bodi ya shiriaka hilo unakuwa na wajumbe
watakaolifanya shirika kuwa na tija.
Nae
Mwakilishi wa Chonga, Abdalla Juma, akitoa maoni yake alisema ipo haja sheria
hiyo inaweka muda maalum wa kumfanya Mkurugenzi kupeleka mahesabu yake kwa mkaguzi
mkuu ndani ya kipindi cha mienzi mitatu badala ya kuacha kuwepo uhuru usiokuwa
na kikomo.
Nae
Mwakilishi wa Kitope, Makame Mshimba Mbarouk, akitoa maoni yake alisema ipo
haja ya serikali kuotumia wataalamu wake kulifanya shirika la meli kuwa lenye
mabadiliko kama inavyotokea katika mamlaka ya uwanja vya ndege Zanzibar.
Alisema
mamlaka ya uwanja wa ndege hivi sasa imeonesha mabadiliko makubwa kutokana na kuwepo uongozi
wenye kuleta tija.
Mwakilishi
wa Wawi, Nassor Saleh, aliipongeza serikali kuleta barazani mswada huo kwani
utazuiya kulifanya shirika hilo
kufanya kazi zake kiholela kamaa lilivyo sasa.
Naye
Mwakilishi wa Micheweni, Shubeit Khamis Faki, akitoa mchango wake alisema
mswada huo unahitaji kuliona shirika litakaloundwa linajiendesha kibiashara
balada ya mtindo wa sasa wa kuwa na majina ya mashirika amabayo hayana tija kwa
taifa.
Nae
Mwakilishi wa viti vya wanawake, Mgeni Hassan, alisema ni vyema wizara ikazingatia
ushauri wa kamati kuona wajumbe wa bodi wanaoteuliwa hawatoki katika serikali
pekee.
MapemaWaziri wa Miundombinu na Mawasiliano,
Rashid Hemed Seif, alisema kuja kwa mswada huo kutaweza kuimarisha kazi za
shirika hilo.
No comments:
Post a Comment