Na Othman Khamis, OMPR
MKURUGENZI
Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF), Ladislaus Mwamanga
amesema mradi wa Tasaf awamu ya tatu unatarajiwa kulenga zaidi katika miradi ya
elimu, afya na maji safi
ili kusaidia zaidi kupunguza umaskini kwa wananchi wanaoishi katika mazingira
magumu.
Hatua
hiyo itakwenda sambamba na uimarishaji wa uongozi katika mifumo ya utekelezaji
wa miradi hiyo ambayo ni muhimu kwa maslahi ya wananchi walio wengi.
Mwamanga
aliyaeleza hayo wakati alipouongoza ujumbe wa viongozi watano wa Tasaf kutoka
makao makuu Dar es Salaam kuzungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
,Balozi Seif Ali Iddi ofisini kwake Vuga.
Alieleza
kwamba Tasaf awamu ya tatu imekusudia kupanua wigo kwa kuendelea kuzishirikisha
Halmashauri za Wilaya kwa upande wa Tanzania
Bara wakati Zanzibar
zitaendelea na hatua ya awali kwa shehia 20 kwa kuzijengea mifumo ya
utekelezaji.
Alisema
Zanzibar imefanikiwa vyema katika utekelezaji wa Tasaf awamu mbili zilizopita
na kuiomba ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ambayo ndio inayoratibu shughuli za
Tasaf Zanzibar kumteua ofisa atakayekuwa na
majukumu ya kuratibu shughuli zote za Tasaf kwa upande wa Zanzibar.
Akitoa
shukrani zake, Balozi Seif alisisitiza suala la kuongezwa taaluma kwa watendaji
wanaosimamia miradi hiyo.
Alisema
kumekuwa na ubadhirifu na matumizi mabovu yaliyokuwa yakifanywa na baadhi ya
wasimamizi wa miradi katika awamu zilizopita tabia ambayo imezorotesha
kutokukamilika au kufa kabisa kwa baadhi ya miradi.
Aliwaasa
watendaji wote wanaopewa jukumu la kusimamia miradi ya Tasaf kujitahidi
kuzingatia uadilifu ili kuepuka ujanja unaobuniwa na baadhi ya wahujumu wa
miradi hiyo kwa maslahi binafsi.
Aliupongeza
Uongozi wa Tasaf kwa uamuzi wake wa kuzingatia zaidi kutoa taaluma kwa
watendaji watakaopewa jukumu la kusimamia miradi ya Tasaf.
No comments:
Post a Comment