Na
Juma Khamis
WANAFUNZI
wa chuo kikuu cha elimu kishiriki Chukwani, bado wanaendelea kutumia maji
ambayo yamechanganyika na chumvi.
Tatizo
hilo ambalo limesababishwa na mabadiliko ya tabianchi, linawaathiri kwa kiasi
kikubwa wanafunzi wa chuo.
Wakizungumza
katika mahafali ya 12 ya chuo hicho jana, wanafunzi hao waliziomba mamlaka
zinazohusika kuingilia kati ili kunusuru hali hiyo ambayo imeanza kuwaathiri.
Kaimu
Mkuu wa chuo hicho, Dk. Hikmany Rashid, alisema tayari uongozi wa chuo
umewasiliana na Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kulishughulikia tatizo hilo.
Changamoto
nyengine ambayo wanafunzi hao walizibainisha ni upungufu wa vitabu katika
maktaba za chuo na tatizo la ajira hasa kwa wahitimu wa fani ya kiarabu na dini
ya kiislamu.
Mapema
akihutubia katika mahafali hayo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Ali Juma
Shamuhuna alikisifu chuo hicho kutokana na mchango wake mkubwa katika
kuimarisha sekta ya elimu nchini kwa kuendeleza kuzalisha walimu wenye ubora.
Alivihimiza
vyuo vikuu kuendelea kufanya tafiti na kuahidi kwamba serikali zote mbili
zitaendelea kuzifanyia kazi tafiti zilizofanywa na watalaamu wa vyuo vikuu.
Aidha
aliwaasa wahitimu kuitumia elimu waliyopata kwa ajili ya kuitumikia jamii,
akisema elimu ni silaha muhimu katika kuleta mageuzi duniani.
Wanafunzi
242 walitunukiwa shahada katika masomo ya sayansi na sanaa.
No comments:
Post a Comment