Na Asya Hassan
WAJAWAZITO 16,277
walijifungua katika hospitali za Mnazimmoja na Mwembeladu mwaka uliopita ambapo
kati yao zaidi
ya 20 walifariki dunia.
Watoto 16,187
walizaliwa katika hospitali hizo mbili ambapo kati yao 724 walifariki dunia kutokana na sababu
mbalimbali.
Aidha wajawazito
waliojifungua wakiwa chini ya umri wa miaka 20 walikuwa 2,045, ambapo hospitali
ya Mnazimmoja walijifungua 1,871 na Mwembeladu 174.
Waliojifungua
wakiwa na umri wa kuanzia miaka 35 walikuwa 2,232, ambapo Mnazimmoja walikuwa
1,738 na Mwembeladu walikuwa 494.
Wajawazito
waliojifungua kwa upasuaji walikuwa 1,679, ambapo Mnazimmoja walikuwa
1,667 na Mwembeladu walikuwa 12 ambapo
walifanya kwa majaribio.
Kwa mujibu wa takwimu
zilizopatikana na gazeti hili, pia zinaonesha wajawazito 75 walijifungulia
nyumbani na baadae kukimbizwa katika hospitali hizo mbili baada ya kupata
matatizo.
Wakizungumza na
gazeti hili baadhi ya wauguzi wa hospitali ya Mnazimmoja ambao hawakutaka majina
yao yachapishwe, walisema idadi ya vifo
vya mama wajawazito imepungua ikilinganishwa na miaka iliyopita.
Hata hivyo,
walisema takwimu zinaonesha vifo kwa ujumla vimepungua kutoka na huduma bora
pamoja na hamasa waliyonayo wajawazito wa kuvitumia vituo vya afya na hospitali
kujifungua.
Waunguzi hao
walisema, hata hivyo tokea kuanza huduma bure kwa wajawazito, wanakabiliwa na
upungufu mkubwa wa vifaa vya kuzalisha pamoja na dawa ambazo mjamzito anapaswa
kupatiwa baada ya kujifungua.
Kwa mfano walisema
wakati mwengine wanakabiliwa na upungufu wa bomba za sindano, ingawa dawa
zinapatikana.
Walisema upungufu
mwengine unaowakabili ni nyuzi za kushonea na sindano zake ambazo ziliopo sasa
ni ndogo, mipira ya kutandika kitandani, mirija ya dripu na glovu.
Waliiomba wizara
ya afya kuongeza vifaa katika wodi za wazazi ili kuzifanya huduma za uzazi
kutolewa kwa ufanisi zaidi.
Katibu wa
hospitali ya Mnazimmoja, Omar Abdalla akizngumza kwa simu alikiri kuwepo kwa
upungufu wa vifaa hivyo, hata hivyo alisema juhudi zinachukuliwa kuhakikisha
upungufu huo unadhibitiwa.
No comments:
Post a Comment