Na Hafsa Golo
WAFANYAKAZI
wa kampuni ya utoaji huduma katika uwanja wa ndege wa Zanzibar (ZAT)
wamelalamika vitendo vya kunyimwa likizo, kwa kile kilichodaiwa na wafanyakazi
hao kuwa kampuni hiyo inajali zaidi maslahi yake.
Mmoja
ya wafanyakazi hao, ambae anafanyakazi kama
mwangalizi ‘supervisor’ (jina tunalihifadhi), alisema hajapewa likizo kwa
vipindi vitano sasa na kila anapoomba anaambiwa asubiri.
Alisema
licha ya kuambiwa asubiri kutoka na sababu mbali mbali ikiwemo kuwepo wageni
wengi, lakini hapewi mafao yake ya kuzuiliwa likizo yake kama
sheria inavyoagiza.
Alisema
kwa mara ya mwisho alipewa likizo mwaka 2007.
“Mimi
nataka kwenda likizo, sina haja ya kulipwa mafao ya kukatishwa likizo yangu,
nataka kupumzika,” alisema.
Alisema
kitendo hicho ni cha uonevu na unyanyasaji lakini pia ni ukiukaji wa haki za
mfanyakazi kisheria.
Lakini
Msaidizi Meneja wa kampuni hiyo, Hassan Mussa alikanusha madai hayo ambapo
alisema kutokana na uelewa alionao katika kampuni hiyo hakuna mfanyakazi
anaeomba likizo akanyimwa kwa sababu ni haki ya
mfanyakazi kisheria hivyo hakuna sababu ya kumnyima.
Alisema
hakuna hata mfanyakazi ambae anadai likizo tano bila kupewa kwa sababu kampuni
inahofia kuwa bila ya mfanyakazi kupewa likizo anaweza kufanya kazi chini ya
kiwango na kusababisha athari kwa kampuni na abiria.
Hata
hivyo, alikiri kwamba kuna baadhi ya wakati
huwataka wafanyakazi wake kuaihirisha likizo yao kutoka kwa kuwepo wageni wengi lakini kipindi hicho kinapomaliza mfanyakazi
huyo hupewa likizo yake.
No comments:
Post a Comment